< Zaburi 106 >

1 Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
2 Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
3 Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
4 Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
5 ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
6 Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
7 Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
8 Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
9 Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
10 Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
11 Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
12 Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
13 Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
14 Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
15 Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
16 Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
17 Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
18 Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
19 Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
20 Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
21 Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
22 miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
23 Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
24 Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
25 Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
26 Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
27 kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
28 Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
29 Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
30 Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
31 Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
32 Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
33 kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
34 Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
35 bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
36 Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
37 Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
39 Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
40 Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
41 Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
42 Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
43 Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
44 Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
45 kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
46 Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
47 Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
48 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.
Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.

< Zaburi 106 >