< Zaburi 106 >

1 Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
ALELUYA. Alabad á Jehová, porque es bueno; porque para siempre [es] su misericordia.
2 Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
¿Quién expresará las valentías de Jehová? ¿[quién] contará sus alabanzas?
3 Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
Dichosos los que guardan juicio, los que hacen justicia en todo tiempo.
4 Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
Acuérdate de mí, oh Jehová, según [tu] benevolencia para con tu pueblo: visítame con tu salud;
5 ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
Para que yo vea el bien de tus escogidos, para que me goce en la alegría de tu gente, y me gloríe con tu heredad.
6 Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
Pecamos con nuestros padres, hicimos iniquidad, hicimos impiedad.
7 Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
Nuestros padres en Egipto no entendieron tus maravillas; no se acordaron de la muchedumbre de tus misericordias; sino que se rebelaron junto á la mar, en el mar Bermejo.
8 Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
Salvólos empero por amor de su nombre, para hacer notoria su fortaleza.
9 Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
Y reprendió al mar Bermejo, y secólo; é hízoles ir por el abismo, como por un desierto.
10 Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
Y salvólos de mano del enemigo, y rescatólos de mano del adversario.
11 Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
Y cubrieron las aguas á sus enemigos: no quedó uno de ellos.
12 Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
Entonces creyeron á sus palabras, y cantaron su alabanza.
13 Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
Apresuráronse, olvidáronse de sus obras; no esperaron en su consejo.
14 Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
Y desearon con ansia en el desierto; y tentaron á Dios en la soledad.
15 Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
Y él les dió lo que pidieron; mas envió flaqueza en sus almas.
16 Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
Tomaron después celo contra Moisés en el campo, [y] contra Aarón el santo de Jehová.
17 Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
Abrióse la tierra, y tragó á Dathán, y cubrió la compañía de Abiram.
18 Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
Y encendióse el fuego en su junta; la llama quemó los impíos.
19 Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
Hicieron becerro en Horeb, y encorváronse á un vaciadizo.
20 Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
Así trocaron su gloria por la imagen de un buey que come hierba.
21 Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
Olvidaron al Dios de su salud, que había hecho grandezas en Egipto;
22 miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
Maravillas en la tierra de Châm, cosas formidables sobre el mar Bermejo.
23 Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
Y trató de destruirlos, á no haberse puesto Moisés su escogido al portillo delante de él, á fin de apartar su ira, para que no [los] destruyese.
24 Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
Empero aborrecieron la tierra deseable: no creyeron á su palabra;
25 Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
Antes murmuraron en sus tiendas, y no oyeron la voz de Jehová.
26 Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
Por lo que alzó su mano á ellos, en orden á postrarlos en el desierto,
27 kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
Y humillar su simiente entre las gentes, y esparcirlos por las tierras.
28 Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
Allegáronse asimismo á Baal-peor, y comieron los sacrificios de los muertos.
29 Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
Y ensañaron [á Dios] con sus obras, y desarrollóse la mortandad en ellos.
30 Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
Entonces se levantó Phinees, é hizo juicio; y se detuvo la plaga.
31 Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
Y fuéle contado á justicia de generación en generación para siempre.
32 Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
También le irritaron en las aguas de Meriba: é hizo mal á Moisés por causa de ellos;
33 kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
Porque hicieron se rebelase su espíritu, como lo expresó con sus labios.
34 Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
No destruyeron los pueblos que Jehová les dijo;
35 bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
Antes se mezclaron con las gentes, y aprendieron sus obras,
36 Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
Y sirvieron á sus ídolos; los cuales les fueron por ruina.
37 Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
Y sacrificaron sus hijos y sus hijas á los demonios;
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
Y derramaron la sangre inocente, la sangre de sus hijos y de sus hijas, que sacrificaron á los ídolos de Canaán: y la tierra fué contaminada con sangre.
39 Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
Contamináronse así con sus obras, y fornicaron con sus hechos.
40 Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
Encendióse por tanto el furor de Jehová sobre su pueblo, y abominó su heredad:
41 Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
Y entrególos en poder de las gentes, y enseñoreáronse de ellos los que los aborrecían.
42 Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
Y sus enemigos los oprimieron, y fueron quebrantados debajo de su mano.
43 Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
Muchas veces los libró; mas ellos se rebelaron á su consejo, y fueron humillados por su maldad.
44 Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
El con todo, miraba cuando estaban en angustia, y oía su clamor:
45 kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
Y acordábase de su pacto con ellos, y arrepentíase conforme á la muchedumbre de sus miseraciones.
46 Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
Hizo asimismo tuviesen de ellos misericordia todos los que los tenían cautivos.
47 Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
Sálvanos, Jehová Dios nuestro, y júntanos de entre las gentes, para que loemos tu santo nombre, para que nos gloriemos en tus alabanzas.
48 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.
Bendito Jehová Dios de Israel, desde el siglo y hasta el siglo: y diga todo el pueblo, Amén. Aleluya.

< Zaburi 106 >