< Zaburi 106 >
1 Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
¡Aleluya! Den gracias a Yavé, Porque Él es bueno, Porque para siempre es su misericordia.
2 Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
¿Quién puede contar las proezas de Yavé? ¿Quién proclama toda su alabanza?
3 Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
¡Dichosos los que guardan recto juicio, Los que practican justicia en todo tiempo!
4 Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
Acuérdate de mí, oh Yavé, Según tu buena voluntad para tu pueblo. Visítame con tu salvación,
5 ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
Para que yo vea el bien de tus escogidos, Para que me regocije por la alegría de tu pueblo, Que me gloríe con tu heredad.
6 Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
Como nuestros antepasados pecamos. Cometimos iniquidad. Nos portamos perversamente.
7 Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
Nuestros antepasados no entendieron tus maravillas en Egipto. No recordaron tus numerosas bondades, Sino se rebelaron junto al mar, en el mar Rojo.
8 Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
Pero Él los salvó por amor a su Nombre Para que fuera evidente su poder.
9 Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
Reprendió al mar Rojo Y lo secó, Y los condujo por las profundidades, Como por un desierto.
10 Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
Así los salvó de [la] mano del que [los] odiaba, Y los redimió de la mano del enemigo.
11 Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
Cubrieron las aguas a sus adversarios, No quedó ni uno de ellos.
12 Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
Entonces creyeron a sus Palabras, Y cantaron su alabanza.
13 Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
Muy pronto olvidaron sus obras. No esperaron su consejo.
14 Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
Con avidez desearon comer en el desierto, Y en lugar despoblado tentaron a ʼElohim.
15 Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
Él les dio lo que pidieron, Pero envió mortandad sobre ellos.
16 Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
Tuvieron envidia de Moisés en el campamento, Y de Aarón, el consagrado a Yavé.
17 Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
Se abrió la tierra Y se tragó a Datán, Y cubrió al grupo de Abiram.
18 Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
Un fuego se encendió contra su grupo. La llama devoró a los perversos.
19 Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
Hicieron un becerro en Horeb. Se postraron ante una imagen de fundición.
20 Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
Así cambiaron la Gloria de ellos Por la imagen de un becerro que come hierba.
21 Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
Olvidaron al ʼEL, su Salvador, Quien hizo grandes cosas en Egipto,
22 miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
Maravillas en la tierra de Cam, Portentos en el mar Rojo.
23 Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
Por tanto Él dijo que los destruiría. Si no fuera porque Moisés su escogido, Se puso en la brecha delante de Él Con la intención de que no los destruyera.
24 Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
Luego despreciaron [la] tierra deseable. No creyeron en la Palabra de Él,
25 Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
Sino murmuraron en sus tiendas. No escucharon la voz de Yavé.
26 Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
Por tanto les juró Que caerían en el desierto,
27 kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
Que dispersaría su descendencia entre las naciones Y los esparciría por las tierras.
28 Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
Se unieron también a Baal-peor Y comieron lo sacrificado a los muertos.
29 Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
Así [lo] provocaron a ira con sus obras, Y una mortandad irrumpió entre ellos.
30 Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
Pero Finees se levantó e intervino, Y la mortandad se detuvo,
31 Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
Y le fue atribuido como justicia Por todas las generaciones para siempre.
32 Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
También [lo] provocaron a ira en las aguas de Meriba, Y salió mal Moisés por causa de ellos,
33 kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
Porque hicieron rebelar su espíritu, Y él habló precipitadamente con sus labios.
34 Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
No destruyeron a los pueblos, Como Yavé les mandó,
35 bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
Sino se mezclaron con gentiles. Aprendieron sus prácticas,
36 Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
Y sirvieron a sus ídolos, Los cuales fueron una trampa.
37 Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
Sacrificaron sus hijos y sus hijas a los demonios
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
Y derramaron sangre inocente, La sangre de sus hijos y de sus hijas, A quienes sacrificaron a los ídolos de Canaán, Y la tierra fue contaminada con la sangre.
39 Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
Así se contaminaron con las prácticas de ellos, Y se prostituyeron con sus hechos.
40 Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
Por tanto la ira de Yavé se encendió contra su pueblo, Y Él repugnó su heredad.
41 Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
Los entregó en [la] mano de los gentiles, Y aquellos que los odiaban gobernaron sobre ellos.
42 Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
Sus enemigos también los oprimieron, Y fueron sometidos bajo su poder.
43 Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
Muchas veces los libró, Pero ellos se rebelaron contra su consejo en su designio, Y así se hundieron en su iniquidad.
44 Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
Sin embargo, Él miraba su angustia Y escuchaba su clamor.
45 kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
Recordaba su Pacto por amor a ellos, Y se compadecía según la grandeza de su misericordia.
46 Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
También promovió que fueran [objeto] de misericordia Por parte de todos los que los tenían cautivos.
47 Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
Oh Yavé, ʼElohim nuestro, sálvanos. Recógenos de entre las naciones, Para que demos gracias a tu santo Nombre Y nos gloriemos en tus alabanzas.
48 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.
¡Bendito sea Yavé, el ʼElohim de Israel, Desde la eternidad hasta la eternidad! Y todo el pueblo diga: ¡Amén! ¡Aleluya!