< Zaburi 106 >
1 Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
¡Alabado sea Yahvé! Dad gracias a Yahvé, porque es bueno, porque su bondad es eterna.
2 Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
¿Quién puede pronunciar los actos poderosos de Yahvé? o declarar plenamente todas sus alabanzas?
3 Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
Dichosos los que guardan la justicia. Dichoso el que hace lo correcto en todo momento.
4 Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
Acuérdate de mí, Yahvé, con el favor que muestras a tu pueblo. Visítame con tu salvación,
5 ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
para que vea la prosperidad de tus elegidos, para que me regocije en la alegría de tu nación, para que me gloríe con tu herencia.
6 Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
Hemos pecado con nuestros padres. Hemos cometido una iniquidad. Hemos hecho maldades.
7 Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
Nuestros padres no entendieron tus maravillas en Egipto. No recordaron la multitud de tus bondades amorosas, pero fueron rebeldes en el mar, incluso en el Mar Rojo.
8 Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
Sin embargo, los salvó por su nombre, para dar a conocer su poderoso poder.
9 Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
También reprendió al Mar Rojo, y se secó; por lo que los condujo a través de las profundidades, como a través de un desierto.
10 Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
Los salvó de la mano del que los odiaba, y los redujo de la mano del enemigo.
11 Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
Las aguas cubrieron a sus adversarios. No quedaba ni uno de ellos.
12 Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
Entonces creyeron en sus palabras. Cantaron sus alabanzas.
13 Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
Pronto olvidaron sus obras. No esperaron su consejo,
14 Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
pero cedió al deseo en el desierto, y puso a prueba a Dios en el páramo.
15 Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
Les concedió su petición, sino que enviaron a su alma la delgadez.
16 Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
También envidiaban a Moisés en el campamento, y Aarón, el santo de Yahvé.
17 Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
La tierra se abrió y se tragó a Datán, y cubrió la compañía de Abiram.
18 Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
Se encendió un fuego en su compañía. La llama quemó a los malvados.
19 Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
Hicieron un becerro en Horeb, y adoraron una imagen fundida.
20 Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
Así intercambiaron su gloria para una imagen de un toro que come hierba.
21 Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
Se olvidaron de Dios, su Salvador, que había hecho grandes cosas en Egipto,
22 miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
obras maravillosas en la tierra de Cam, y cosas impresionantes junto al Mar Rojo.
23 Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
Por eso dijo que los destruiría, si Moisés, su elegido, no se hubiera puesto delante de él en la brecha, para alejar su ira, para que no los destruya.
24 Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
Sí, despreciaron la tierra agradable. No creyeron en su palabra,
25 Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
sino que murmuraban en sus tiendas, y no escucharon la voz de Yahvé.
26 Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
Por eso les juró que los derrocaría en el desierto,
27 kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
que él derrocaría a su descendencia entre las naciones, y dispersarlos en las tierras.
28 Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
También se unieron a Baal Peor, y comieron los sacrificios de los muertos.
29 Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
Así le provocaron la ira con sus actos. La peste se abatió sobre ellos.
30 Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
Entonces Finees se levantó y ejecutó el juicio, por lo que la plaga fue detenida.
31 Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
Eso se le acreditó como justicia, para todas las generaciones venideras.
32 Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
También lo enfurecieron en las aguas de Meribá, por lo que Moisés se preocupó por ellos;
33 kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
porque eran rebeldes a su espíritu, habló precipitadamente con los labios.
34 Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
No destruyeron los pueblos, como les ordenó Yahvé,
35 bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
sino que se mezclaron con las naciones, y aprendieron sus obras.
36 Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
Servían a sus ídolos, que se convirtió en una trampa para ellos.
37 Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
Sí, sacrificaron a sus hijos e hijas a los demonios.
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
Derramaron sangre inocente, incluso la sangre de sus hijos y de sus hijas, que sacrificaron a los ídolos de Canaán. La tierra estaba contaminada con sangre.
39 Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
Así se contaminaron con sus obras, y se prostituyeron en sus actos.
40 Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
Por eso Yahvé ardió de ira contra su pueblo. Aborrecía su herencia.
41 Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
Los entregó en manos de las naciones. Los que los odiaban los gobernaban.
42 Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
Sus enemigos también los oprimieron. Fueron sometidos bajo su mano.
43 Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
Los rescató muchas veces, pero fueron rebeldes en su consejo, y fueron abatidos en su iniquidad.
44 Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
Sin embargo, él consideró su angustia, cuando escuchó su grito.
45 kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
Se acordó por ellos de su pacto, y se arrepintió según la multitud de sus bondades.
46 Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
También hizo que se compadecieran de ellos por todos aquellos que los llevaron cautivos.
47 Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
Sálvanos, Yahvé, nuestro Dios, reunirnos de entre las naciones, para dar gracias a tu santo nombre, ¡para triunfar en tu alabanza!
48 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.
Bendito sea Yahvé, el Dios de Israel, ¡desde la eternidad hasta la eternidad! Que todo el pueblo diga: “Amén”. ¡Alabado sea Yah!