< Zaburi 106 >

1 Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Alleluia. Confitemini Domino quoniam bonus: quoniam in sæculum misericordia eius.
2 Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
Quis loquetur potentias Domini, auditas faciet omnes laudes eius?
3 Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
Beati, qui custodiunt iudicium, et faciunt iustitiam in omni tempore.
4 Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
Memento nostri Domine in beneplacito populi tui: visita nos in salutari tuo:
5 ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
Ad videndum in bonitate electorum tuorum, ad lætandum in lætitia gentis tuæ: ut lauderis cum hereditate tua.
6 Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
Peccavimus cum patribus nostris: iniuste egimus, iniquitatem fecimus.
7 Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
Patres nostri in Ægypto non intellexerunt mirabilia tua: non fuerunt memores multitudinis misericordiæ tuæ. Et irritaverunt ascendentes in mare, Mare rubrum.
8 Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
Et salvavit eos propter nomen suum: ut notam faceret potentiam suam.
9 Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
Et increpuit Mare rubrum, et exiccatum est: et deduxit eos in abyssis sicut in deserto.
10 Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
Et salvavit eos de manu odientium: et redemit eos de manu inimici.
11 Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
Et operuit aqua tribulantes eos: unus ex eis non remansit.
12 Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
Et crediderunt verbis eius: et laudaverunt laudem eius.
13 Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
Cito fecerunt, obliti sunt operum eius: et non sustinuerunt consilium eius.
14 Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
Et concupierunt concupiscentiam in deserto: et tentaverunt Deum in inaquoso
15 Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
Et dedit eis petitionem ipsorum: et misit saturitatem in animas eorum.
16 Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
Et irritaverunt Moysen in castris: Aaron sanctum Domini.
17 Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
Aperta est terra, et deglutivit Dathan: et operuit super congregationem Abiron.
18 Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
Et exarsit ignis in synagoga eorum: flamma combussit peccatores.
19 Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
Et fecerunt vitulum in Horeb: et adoraverunt sculptile.
20 Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
Et mutaverunt gloriam suam in similitudinem vituli comedentis fœnum.
21 Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
Obliti sunt Deum, qui salvavit eos, qui fecit magnalia in Ægypto,
22 miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
mirabilia in Terra Cham: terribilia in mari rubro.
23 Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
Et dixit ut disperderet eos: si non Moyses electus eius stetisset in confractione in conspectu eius: Ut averteret iram eius ne disperderet eos:
24 Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
et pro nihilo habuerunt terram desiderabilem: Non crediderunt verbo eius,
25 Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
et murmuraverunt in tabernaculis suis: non exaudierunt vocem Domini.
26 Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
Et elevavit manum suam super eos: ut prosterneret eos in deserto:
27 kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
Et ut deiiceret semen eorum in Nationibus: et dispergeret eos in regionibus.
28 Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
Et initiati sunt Beelphegor: et comederunt sacrificia mortuorum.
29 Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
Et irritaverunt eum in adinventionibus suis: et multiplicata est in eis ruina.
30 Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
Et stetit Phinees, et placavit: et cessavit quassatio.
31 Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
Et reputatum est ei in iustitiam, in generationem et generationem usque in sempiternum.
32 Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
Et irritaverunt eum ad Aquas contradictionis: et vexatus est Moyses propter eos:
33 kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
quia exacerbaverunt spiritum eius. Et distinxit in labiis suis:
34 Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
non disperdiderunt gentes, quas dixit Dominus illis.
35 bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
Et commisti sunt inter gentes, et didicerunt opera eorum:
36 Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
et servierunt sculptilibus eorum: et factum est illis in scandalum.
37 Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
Et immolaverunt filios suos, et filias suas dæmoniis.
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
Et effuderunt sanguinem innocentem: sanguinem filiorum suorum et filiarum suarum, quas sacrificaverunt sculptilibus Chanaan. Et infecta est terra in sanguinibus,
39 Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
et contaminata est in operibus eorum: et fornicati sunt in adinventionibus suis.
40 Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
Et iratus est furore Dominus in populum suum: et abominatus est hereditatem suam.
41 Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
Et tradidit eos in manus gentium: et dominati sunt eorum qui oderunt eos.
42 Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
Et tribulaverunt eos inimici eorum, et humiliati sunt sub manibus eorum:
43 Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
sæpe liberavit eos. Ipsi autem exacerbaverunt eum in consilio suo: et humiliati sunt in iniquitatibus suis.
44 Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
Et vidit cum tribularentur: et audivit orationem eorum.
45 kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
Et memor fuit testamenti sui: et pœnituit eum secundum multitudinem misericordiæ suæ.
46 Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
Et dedit eos in misericordias in conspectu omnium qui ceperant eos.
47 Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
Salvos nos fac Domine Deus noster: et congrega nos de Nationibus: Ut confiteamur nomini sancto tuo: et gloriemur in laude tua.
48 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.
Benedictus Dominus Deus Israel a sæculo et usque in sæculum: et dicet omnis populus: Fiat, fiat.

< Zaburi 106 >