< Zaburi 106 >
1 Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
ヱホバをほめたたへヱホバに感謝せよ そのめぐみはふかくその憐憫はかぎりなし
2 Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
たれかヱホバの力ある事跡をかたり その讃べきことを悉とくいひあらはし得んや
3 Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
審判をまもる人々つねに正義をおこなふ者はさいはひなり
4 Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
ヱホバよなんぢの民にたまふ惠をもて我をおぼえ なんぢの救をもてわれに臨みたまへ
5 ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
さらば我なんぢの撰びたまへる者のさいはひを見 なんぢの國の歓喜をよろこび なんぢの嗣業とともに誇ることをせん
6 Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
われら列祖とともに罪ををかせり 我儕よこしまをなし惡をおこなへり
7 Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
われらの列祖はなんぢがエジプトにてなしたまへる奇しき事跡をさとらず 汝のあはれみの豊かなるを心にとめず 海のほとり即ち紅海のほとりにて逆きたり
8 Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
されどヱホバはその名のゆゑをもて彼等をすくひたまへり こは大なる能力をしらしめんとてなり
9 Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
また紅海を叱咤したまひたれば乾きたり かくて民をみちびきて野をゆくがごとくに淵をすぎしめ
10 Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
恨むるものの手よりかれらをすくひ 仇の手よりかれらを贖ひたまへり
11 Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
水その敵をおほひたればその一人だにのこりし者なかりき
12 Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
このとき彼等そのみことばを信じその頌美をうたへり
13 Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
彼等しばしがほどにその事跡をわすれその訓誨をまたず
14 Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
野にていたくむさぼり荒野にて神をこころみたりき
15 Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
ヱホバはかれらの願欲をかなへたまひしかど その霊魂をやせしめたまへり
16 Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
たみは營のうちにてモーセを嫉みヱホパの聖者アロンをねたみしかば
17 Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
地ひらけてダタンを呑みアビラムの黨類をおほひ
18 Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
火はこのともがらの中にもえおこり熖はあしき者をやきつくせり
19 Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
かれらはホレブの山にて犢をつくり鑄たる像ををがみたり
20 Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
かくの如くおのが榮光をかへて草をくらふ牛のかたちに似す
21 Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
救主なる神はエジプトにて大なるわざをなし
22 miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
ハムの地にて奇しき事跡をなし紅海のほとりにて懼るべきことを爲たまへり かれは斯る神をわすれたり
23 Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
この故にヱホバかれらを亡さんと宣まへり されど神のえらみたまへる者モーセやぶれの間隙にありてその前にたちその烈怒をひきかへして滅亡をまぬかれしめたり
24 Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
かれら美しき地を蔑しそのみことばを信ぜず
25 Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
剰さへその幕屋にてつぶやきヱホバの聲をもきかざりき
26 Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
この故に手をあげて彼等にむかひたまへり これ野にてかれらを斃れしめんとし
27 kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
又もろもろの國のうちにてその裔をたふれしめ もろもろの地にかれらを散さんとしたまへるなり
28 Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
彼らはバアルベオルにつきて死るものの祭物をくらひたり
29 Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
斯のごとくその行爲をもてヱホバの烈怒をひきいだしければえやみ侵しいりたり
30 Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
そのときピネハスたちて裁判をなせり かくて疫癘はやみぬ
31 Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
ピネハスは萬代までとこしへにこのことを義とせられたり
32 Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
民メリバの水のほとりにてヱホバの烈怒をひきおこししかば かれらの故によりてモーセも禍害にあへり
33 kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
かれら神の霊にそむきしかばモーセその口唇にて妄にものいひたればなり
34 Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
かれらはヱホバの命じたまへる事にしたがはずしてもろもろの民をほろぼさず
35 bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
反てもろもろの國人とまじりをりてその行爲にならひ
36 Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
おのが羂となりしその偶像につかへたり
37 Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
かれらはその子女を鬼にささぐ
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
罪なき血すなはちカナンの偶像にささげたる己がむすこむすめの血をながしぬ 斯てくには血にてけがされたり
39 Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
またそのわざは自己をけがし そのおこなふところは姦淫なり
40 Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
このゆゑにヱホバの怒その民にむかひて起り その嗣業をにくみて
41 Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
かれらをもろもろの國の手にわたしたまへり 彼等はおのれを恨るものに制へられ
42 Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
おのれの仇にしへたげられ その手の下にうちふせられたり
43 Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
ヱホバはしばしば助けたまひしかどかれらは謀略をまうけて逆き そのよこしまに卑くせられたり
44 Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
されどヱホバはかれらの哭聲をききたまひしとき その患難をかへりみ
45 kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
その契約をかれらの爲におもひいだし その憐憫のゆたかなるにより聖意をかへさせ給ひて
46 Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
かれらを己がとりこにせられたる者どもに憐まるることを得しめたまへり
47 Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
われらの神ヱホバよ われらをすくひて列邦のなかより取集めたまへ われらは聖名に謝し なんぢのほむべき事をほこらん
48 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.
イスラエルの神ヱホバはとこしへより永遠までほむべきかな すべての民はアーメンととなふべし ヱホバを讃稱へよ