< Zaburi 106 >
1 Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Celebrate il Signore, perché è buono, perché eterna è la sua misericordia. Alleluia.
2 Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
Chi può narrare i prodigi del Signore, far risuonare tutta la sua lode?
3 Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
Beati coloro che agiscono con giustizia e praticano il diritto in ogni tempo.
4 Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
Ricordati di noi, Signore, per amore del tuo popolo, visitaci con la tua salvezza,
5 ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
perché vediamo la felicità dei tuoi eletti, godiamo della gioia del tuo popolo, ci gloriamo con la tua eredità.
6 Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
Abbiamo peccato come i nostri padri, abbiamo fatto il male, siamo stati empi.
7 Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
I nostri padri in Egitto non compresero i tuoi prodigi, non ricordarono tanti tuoi benefici e si ribellarono presso il mare, presso il mar Rosso.
8 Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
Ma Dio li salvò per il suo nome, per manifestare la sua potenza.
9 Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
Minacciò il mar Rosso e fu disseccato, li condusse tra i flutti come per un deserto;
10 Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
li salvò dalla mano di chi li odiava, li riscattò dalla mano del nemico.
11 Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
L'acqua sommerse i loro avversari; nessuno di essi sopravvisse.
12 Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
Allora credettero alle sue parole e cantarono la sua lode.
13 Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
Ma presto dimenticarono le sue opere, non ebbero fiducia nel suo disegno,
14 Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
arsero di brame nel deserto, e tentarono Dio nella steppa.
15 Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
Concesse loro quanto domandavano e saziò la loro ingordigia.
16 Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
Divennero gelosi di Mosè negli accampamenti, e di Aronne, il consacrato del Signore.
17 Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
Allora si aprì la terra e inghiottì Datan, e seppellì l'assemblea di Abiron.
18 Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
Divampò il fuoco nella loro fazione e la fiamma divorò i ribelli.
19 Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
Si fabbricarono un vitello sull'Oreb, si prostrarono a un'immagine di metallo fuso;
20 Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
scambiarono la loro gloria con la figura di un toro che mangia fieno.
21 Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
Dimenticarono Dio che li aveva salvati, che aveva operato in Egitto cose grandi,
22 miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
prodigi nel paese di Cam, cose terribili presso il mar Rosso.
23 Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
E aveva gia deciso di sterminarli, se Mosè suo eletto non fosse stato sulla breccia di fronte a lui, per stornare la sua collera dallo sterminio.
24 Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
Rifiutarono un paese di delizie, non credettero alla sua parola.
25 Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
Mormorarono nelle loro tende, non ascoltarono la voce del Signore.
26 Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
Egli alzò la mano su di loro giurando di abbatterli nel deserto,
27 kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
di disperdere i loro discendenti tra le genti e disseminarli per il paese.
28 Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
Si asservirono a Baal-Peor e mangiarono i sacrifici dei morti,
29 Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
provocarono Dio con tali azioni e tra essi scoppiò una pestilenza.
30 Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
Ma Finees si alzò e si fece giudice, allora cessò la peste
31 Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
e gli fu computato a giustizia presso ogni generazione, sempre.
32 Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
Lo irritarono anche alle acque di Meriba e Mosè fu punito per causa loro,
33 kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
perché avevano inasprito l'animo suo ed egli disse parole insipienti.
34 Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
Non sterminarono i popoli come aveva ordinato il Signore,
35 bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
ma si mescolarono con le nazioni e impararono le opere loro.
36 Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
Servirono i loro idoli e questi furono per loro un tranello.
37 Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
Immolarono i loro figli e le loro figlie agli dei falsi.
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
Versarono sangue innocente, il sangue dei figli e delle figlie sacrificati agli idoli di Canaan; la terra fu profanata dal sangue,
39 Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
si contaminarono con le opere loro, si macchiarono con i loro misfatti.
40 Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
L'ira del Signore si accese contro il suo popolo, ebbe in orrore il suo possesso;
41 Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
e li diede in balìa dei popoli, li dominarono i loro avversari,
42 Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
li oppressero i loro nemici e dovettero piegarsi sotto la loro mano.
43 Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
Molte volte li aveva liberati; ma essi si ostinarono nei loro disegni e per le loro iniquità furono abbattuti.
44 Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
Pure, egli guardò alla loro angoscia quando udì il loro grido.
45 kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
Si ricordò della sua alleanza con loro, si mosse a pietà per il suo grande amore.
46 Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
Fece loro trovare grazia presso quanti li avevano deportati.
47 Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
Salvaci, Signore Dio nostro, e raccoglici di mezzo ai popoli, perché proclamiamo il tuo santo nome e ci gloriamo della tua lode.
48 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.
Benedetto il Signore, Dio d'Israele da sempre, per sempre. Tutto il popolo dica: Amen.