< Zaburi 106 >

1 Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Hallelujah! Danket dem HERRN, denn er ist gütig, seine Gnade währt ewiglich!
2 Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
Wer kann die Machttaten des HERRN beschreiben und allen seinen Ruhm verkünden?
3 Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
Wohl denen, die das Recht beachten, die Gerechtigkeit üben allezeit!
4 Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
Gedenke meiner, o HERR, aus Gnaden gegen dein Volk, suche mich heim mit deinem Heil,
5 ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
daß ich einen Einblick bekomme in das Wohlergehen deiner Auserwählten, mich freue an der Freude deines Volkes und mich deines Erbteils rühme.
6 Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
Wir haben gesündigt samt unsern Vätern, wir haben verkehrt gehandelt, wir haben gefrevelt.
7 Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
Unsre Väter in Ägypten hatten nicht acht auf deine Wunder, sie gedachten nicht an die Größe deiner Güte und waren widerspenstig am Meer, am Schilfmeer.
8 Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
Aber er half ihnen um seines Namens willen, um seine Stärke kundzutun.
9 Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
Und er bedrohte das Schilfmeer, daß es vertrocknete, und ließ sie durch die Tiefen gehen wie auf einer Steppe.
10 Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
Und er rettete sie von der Hand des Hassers und erlöste sie aus der Hand des Feindes.
11 Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
Und das Wasser bedeckte ihre Bedränger, nicht einer von ihnen blieb übrig.
12 Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
Da glaubten sie seinen Worten und sangen sein Lob.
13 Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
Aber sie vergaßen seine Werke bald, sie warteten nicht auf seinen Rat,
14 Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
sondern ließen sich gelüsten in der Wüste und versuchten Gott in der Einöde.
15 Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
Und er gab ihnen, was sie forderten, sandte aber eine Seuche unter sie.
16 Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
Und sie wurden eifersüchtig auf Mose im Lager, auf Aaron, den Heiligen des HERRN.
17 Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
Da tat sich die Erde auf und verschlang Datan und bedeckte die Rotte Abirams;
18 Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
und Feuer verzehrte ihre Rotte, die Flamme versengte die Gottlosen.
19 Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
Sie machten ein Kalb am Horeb und warfen sich nieder vor dem gegossenen Bild.
20 Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
Sie vertauschten ihre Herrlichkeit gegen das Abbild eines Stiers, der Gras frißt.
21 Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
Sie vergaßen Gottes, ihres Retters, der große Dinge in Ägypten getan,
22 miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
Wunder im Lande Hams, Furchtbares am Schilfmeer.
23 Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
Und er gedachte sie zu vertilgen, wenn nicht Mose, sein Auserwählter, in den Riß getreten wäre vor seinem Angesicht, um seinen Grimm abzuwenden, daß er sie nicht vertilgte.
24 Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
Sie verachteten das liebliche Land, sie glaubten seinem Worte nicht.
25 Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
Und sie murrten in ihren Zelten, sie gehorchten nicht der Stimme des HERRN.
26 Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
Da erhob er seine Hand [und schwur], sie niederzustrecken in der Wüste
27 kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
und ihren Samen unter die Nationen zu werfen und sie zu zerstreuen in die Länder.
28 Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
Und sie hängten sich an den Baal-Peor und aßen Opfer der toten [Götzen],
29 Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
und sie erzürnten ihn mit ihrem Tun; da brach die Plage unter ihnen aus.
30 Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
Aber Pinehas trat auf und übte Gericht, so daß die Plage aufgehalten ward.
31 Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
Das wurde ihm zur Gerechtigkeit gerechnet auf alle Geschlechter, in Ewigkeit.
32 Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
Und sie erzürnten ihn am Haderwasser, und es erging Mose übel um ihretwillen.
33 kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
Denn sie betrübten seinen Geist, und er redete unbedacht mit seinen Lippen.
34 Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
Sie vertilgten die Völker nicht, von denen der HERR ihnen gesagt hatte;
35 bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
sondern ließen sich ein mit den Heiden und lernten ihre Weise.
36 Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
Und sie dienten ihren Götzen, und diese wurden ihnen zum Fallstrick.
37 Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
Und sie opferten ihre Söhne und ihre Töchter den bösen Geistern.
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
Und sie vergossen unschuldiges Blut, das Blut ihrer Söhne und ihrer Töchter, welche sie den Götzen Kanaans opferten, und so wurde das Land durch Blutschulden entweiht.
39 Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
Und sie befleckten sich mit ihren Werken und hurten mit ihrem Tun.
40 Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
Da entbrannte der Zorn des HERRN wider sein Volk, und er faßte einen Abscheu gegen sein Erbe.
41 Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
Und er gab sie in die Hand der Nationen, daß ihre Hasser über sie herrschten.
42 Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
Und ihre Feinde bedrückten sie, und sie wurden gedemütigt unter ihre Hand.
43 Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
Er errettete sie oftmals; aber sie widerstrebten ihm mit ihren Anschlägen und kamen herunter durch eigene Schuld.
44 Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
Aber er sah ihre Not an, als er ihr Schreien hörte,
45 kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
und gedachte seines Bundes mit ihnen und empfand Mitleid nach seiner großen Huld
46 Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
und ließ sie Erbarmen finden bei denen, die sie gefangen hielten.
47 Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
Hilf uns, HERR, unser Gott, sammle uns aus den Heiden, daß wir deinem heiligen Namen danken und uns glücklich preisen, zu deinem Ruhm!
48 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.
Gelobt sei der HERR, der Gott Israels, von Ewigkeit zu Ewigkeit, und alles Volk soll sagen: Amen! Hallelujah!

< Zaburi 106 >