< Zaburi 106 >
1 Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Louez l'Éternel! Célébrez l'Éternel, car il est bon, car sa miséricorde demeure à toujours!
2 Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
Qui pourrait raconter les hauts faits de l'Éternel et faire entendre toutes ses louanges?
3 Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
Heureux ceux qui observent ce qui est droit, qui font en tout temps ce qui est juste!
4 Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
Éternel, souviens-toi de moi, dans ta bienveillance envers ton peuple; fais venir à moi ton salut;
5 ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
Afin que je voie le bonheur de tes élus, que je me réjouisse de la joie de ton peuple, et que je me glorifie avec ton héritage.
6 Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
Nous et nos pères, nous avons péché; nous avons agi avec perversité; nous avons mal fait.
7 Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
Nos pères en Égypte ne furent pas attentifs à tes merveilles; ils ne se souvinrent point de la multitude de tes bontés; mais ils furent rebelles auprès de la mer, vers la mer Rouge.
8 Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
Et il les sauva pour l'amour de son nom, afin de faire connaître sa puissance.
9 Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
Il tança la mer Rouge, et elle fut à sec; et il les conduisit par les abîmes comme par le désert.
10 Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
Il les sauva des mains de l'adversaire, et les racheta des mains de l'ennemi.
11 Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
Les eaux couvrirent leurs oppresseurs; il n'en resta pas un seul.
12 Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
Alors ils crurent à ses paroles, et ils chantèrent sa louange.
13 Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
Bientôt ils oublièrent ses œuvres; ils ne s'attendirent point à ses desseins.
14 Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
Ils s'éprirent de convoitise dans le désert, et tentèrent Dieu dans la solitude.
15 Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
Alors il leur accorda leur demande; mais il envoya sur eux la consomption.
16 Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
Ils furent jaloux de Moïse dans le camp, et d'Aaron, le saint de l'Éternel.
17 Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
La terre s'ouvrit, et engloutit Dathan, et couvrit la troupe d'Abiram.
18 Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
Le feu s'alluma dans leur assemblée; la flamme consuma les méchants.
19 Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
Ils firent un veau en Horeb, et se prosternèrent devant une image de fonte.
20 Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
Ils échangèrent leur gloire contre la figure du bœuf qui mange l'herbe.
21 Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
Ils oublièrent Dieu, leur libérateur, qui avait fait de grandes choses en Égypte,
22 miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
Des choses merveilleuses au pays de Cham, et des choses terribles sur la mer Rouge.
23 Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
Et il parlait de les détruire, si Moïse, son élu, ne se fût mis à la brèche devant lui, pour détourner sa colère, afin qu'il ne les détruisît pas.
24 Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
Ils méprisèrent la terre désirable; ils ne crurent point à sa parole.
25 Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
Ils murmurèrent dans leurs tentes; ils n'écoutèrent point la voix de l'Éternel.
26 Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
Alors il leur fit serment de les faire tomber dans le désert,
27 kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
De faire tomber leur postérité entre les nations, de les disperser dans tous les pays.
28 Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
Ils s'attachèrent à Baal-Péor, et mangèrent les sacrifices des morts.
29 Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
Ils irritèrent Dieu par leurs actions, tellement qu'une plaie fit irruption parmi eux.
30 Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
Mais Phinées se présenta et fit justice, et la plaie fut arrêtée.
31 Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
Et cela lui fut imputé à justice, dans tous les âges, à perpétuité.
32 Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
Ils l'irritèrent aussi près des eaux de Mériba; et il en arriva du mal à Moïse à cause d'eux.
33 kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
Car ils résistèrent à son esprit, et il parla légèrement de ses lèvres.
34 Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
Ils ne détruisirent pas les peuples, que l'Éternel leur avait dit de détruire.
35 bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
Mais ils se mêlèrent avec les nations, et ils apprirent leurs œuvres.
36 Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
Ils servirent leurs idoles, qui furent pour eux un piège;
37 Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
Et ils sacrifièrent aux démons leurs fils et leurs filles.
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
Ils répandirent le sang innocent, le sang de leurs fils et de leurs filles, qu'ils sacrifièrent aux idoles de Canaan; et le pays fut profané par ces meurtres.
39 Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
Ils se souillèrent par leurs œuvres, et se prostituèrent par leurs actions.
40 Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
Et la colère de l'Éternel s'alluma contre son peuple; il eut en abomination son héritage.
41 Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
Il les livra entre les mains des nations; ceux qui les haïssaient, dominèrent sur eux.
42 Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
Leurs ennemis les opprimèrent, et ils furent humiliés sous leur main.
43 Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
Maintes fois il les délivra; mais ils se montraient rebelles dans leurs desseins, et se perdaient par leur iniquité.
44 Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
Toutefois, il les a regardés dans leur détresse, quand il entendait leur cri.
45 kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
Il s'est souvenu en leur faveur de son alliance, et s'est repenti selon la grandeur de sa miséricorde.
46 Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
Il leur a fait trouver compassion auprès de tous ceux qui les tenaient captifs.
47 Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
Sauve-nous, Éternel, notre Dieu, et rassemble-nous d'entre les nations, afin que nous célébrions ton saint nom, et que nous nous glorifiions dans tes louanges.
48 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.
Béni soit l'Éternel, le Dieu d'Israël, de siècle en siècle, et que tout le peuple dise: Amen! Louez l'Éternel!