< Zaburi 106 >
1 Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Alleluia! Célébrez Yahweh, car il est bon, car sa miséricorde est éternelle.
2 Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
Qui dira les hauts faits de Yahweh! Qui publiera toute sa gloire?
3 Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
Heureux ceux qui observent la loi, qui accomplissent la justice en tout temps!
4 Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
Souviens-toi de moi, Yahweh, dans ta bonté pour ton peuple, visite-moi avec ton secours,
5 ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
afin que je voie le bonheur de tes élus, que je me réjouisse de la joie de ton peuple, et que je me glorifie avec ton héritage.
6 Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
Nous avons péché comme nos pères, nous avons commis l’iniquité, nous avons fait le mal.
7 Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
Nos pères en Égypte n’eurent pas d’égard à tes prodiges, ils ne se souvinrent pas de la multitude de tes grâces, ils se sont révoltés à la mer, à la mer Rouge.
8 Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
Il les sauva pourtant à cause de son nom, pour faire éclater sa puissance.
9 Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
Il menaça la mer Rouge, et elle se dessécha; et il les fit marcher à travers l’abîme comme dans un désert.
10 Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
Il les sauva de la main de celui qui les haïssait, il les délivra de la main de l’oppresseur.
11 Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
Les flots couvrirent leurs adversaires, pas un seul n’échappa.
12 Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
Ils crurent alors à ses paroles, ils chantèrent ses louanges.
13 Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
Mais ils oublièrent bientôt ses œuvres, ils n’attendirent pas qu’il exécutât ses desseins.
14 Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
Ils furent pris de convoitise dans le désert, et ils tentèrent Dieu dans la solitude.
15 Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
Il leur accorda ce qu’ils demandaient, mais il les frappa de consomption.
16 Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
Puis ils furent jaloux de Moïse dans le camp, et d’Aaron, le saint de Yahweh.
17 Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
La terre s’ouvrit et engloutit Dathan, et elle se referma sur la troupe d’Abiron;
18 Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
Le feu dévora leur troupe, la flamme consuma les méchants.
19 Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
Ils firent un veau au mont Horeb, ils se prosternèrent devant une image de métal fondu;
20 Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
Ils échangèrent leur gloire contre la figure d’un bœuf qui mange l’herbe.
21 Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
Ils oublièrent Dieu, leur sauveur, qui avait fait de grandes choses en Égypte,
22 miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
des miracles dans le pays de Cham, des prodiges à la mer Rouge.
23 Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
Il parlait de les exterminer, si Moïse, son élu, ne se fût tenu sur la brèche devant lui, pour empêcher sa colère de les détruire.
24 Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
Ils dédaignèrent la terre de délices, ils ne crurent pas à la parole de Yahweh;
25 Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
ils murmurèrent dans leurs tentes, et n’obéirent pas à sa voix.
26 Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
Alors il leva la main contre eux, jurant de les faire périr dans le désert,
27 kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
de faire périr leur race parmi les nations, et de les disperser en d’autres contrées.
28 Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
Ils s’attachèrent à Béelphégor et mangèrent des victimes offertes aux morts.
29 Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
Ils irritèrent Yahweh par leurs actions, et un fléau fit irruption parmi eux.
30 Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
Phinées se leva et donna satisfaction, et le fléau fut arrêté.
31 Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
Cette action fut imputée à justice, d’âge en âge, à jamais.
32 Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
Ils irritèrent Yahweh aux eaux de Mériba, et Moïse eut à souffrir à cause d’eux;
33 kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
car ils aigrirent son esprit, et il prononça des paroles inconsidérées.
34 Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
Ils n’exterminèrent point les peuples que Yahweh leur avait ordonné de détruire.
35 bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
Ils se mêlèrent aux nations, et ils apprirent leurs œuvres.
36 Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
Ils servirent leurs idoles, qui furent pour eux un piège.
37 Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
Ils immolèrent leurs fils et leurs filles aux démons.
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
Ils versèrent le sang innocent, le sang de leurs fils et de leurs filles, qu’ils sacrifiaient aux idoles de Chanaan; et le pays fut profané par des meurtres.
39 Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
Ils se souillèrent par leurs œuvres, ils se prostituèrent par leurs actions.
40 Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
La colère de Yahweh s’alluma contre son peuple, et il prit en horreur son héritage.
41 Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
Il les livra entre les mains des nations, ceux qui les haïssaient dominèrent sur eux.
42 Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
Leurs ennemis les opprimèrent, et ils furent humiliés sous leur main.
43 Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
Bien des fois il les délivra, mais ils furent rebelles dans leurs desseins, et se perdirent par leurs iniquités.
44 Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
Néanmoins, il regarda leur détresse, lorsqu’il entendit leurs supplications.
45 kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
Il se souvint en leur faveur de son alliance, il eut pitié d’eux selon sa grande bonté,
46 Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
et il en fit l’objet de ses miséricordes, devant tous ceux qui les tenaient captifs.
47 Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
Sauve-nous Yahweh, notre Dieu, et rassemble-nous du milieu des nations, afin que nous célébrions ton saint nom, et que nous mettions notre gloire à te louer.
48 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.
Béni soit Yahweh, Dieu d’Israël, d’éternité en éternité! Et que tout le peuple dise: Amen! Alleluia! Psaumes Livres