< Zaburi 106 >

1 Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
to boast: praise LORD to give thanks to/for LORD for be pleasing for to/for forever: enduring kindness his
2 Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
who? to speak might LORD to hear: proclaim all praise his
3 Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
blessed to keep: obey justice to make: do righteousness in/on/with all time
4 Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
to remember me LORD in/on/with acceptance people your to reckon: visit me in/on/with salvation your
5 ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
to/for to see: enjoy in/on/with welfare chosen your to/for to rejoice in/on/with joy nation your to/for to boast: boast with inheritance your
6 Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
to sin with father our to pervert be wicked
7 Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
father our in/on/with Egypt not be prudent to wonder your not to remember [obj] abundance kindness your and to rebel upon sea in/on/with sea Red (Sea)
8 Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
and to save them because name his to/for to know [obj] might his
9 Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
and to rebuke in/on/with sea Red (Sea) and to dry and to go: take them in/on/with abyss like/as wilderness
10 Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
and to save them from hand: power to hate and to redeem: redeem them from hand: power enemy
11 Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
and to cover water enemy their one from them not to remain
12 Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
and be faithful in/on/with word his to sing praise his
13 Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
to hasten to forget deed: work his not to wait to/for counsel his
14 Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
and to desire desire in/on/with wilderness and to test God in/on/with wilderness
15 Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
and to give: give to/for them petition their and to send: depart leanness in/on/with soul: myself their
16 Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
and be jealous to/for Moses in/on/with camp to/for Aaron holy: saint LORD
17 Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
to open land: country/planet and to swallow up Dathan and to cover upon congregation Abiram
18 Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
and to burn: burn fire in/on/with congregation their flame to kindle wicked
19 Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
to make calf in/on/with Horeb and to bow to/for liquid
20 Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
and to change [obj] glory their in/on/with pattern cattle to eat vegetation
21 Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
to forget God to save them to make: do great: large in/on/with Egypt
22 miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
to wonder in/on/with land: country/planet Ham to fear: revere upon sea Red (Sea)
23 Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
and to say to/for to destroy them unless Moses chosen his to stand: stand in/on/with breach to/for face: before his to/for to return: turn back rage his from to ruin
24 Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
and to reject in/on/with land: country/planet desire not be faithful to/for word: promised his
25 Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
and to grumble in/on/with tent their not to hear: obey in/on/with voice LORD
26 Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
and to lift: vow hand: vow his to/for them to/for to fall: fall [obj] them in/on/with wilderness
27 kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
and to/for to fall: fall seed: children their in/on/with nation and to/for to scatter them in/on/with land: country/planet
28 Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
and to join to/for Baal of Peor Baal of Peor and to eat sacrifice to die
29 Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
and to provoke in/on/with deed their and to break through in/on/with them plague
30 Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
and to stand: stand Phinehas and to pray and to restrain [the] plague
31 Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
and to devise: count to/for him to/for righteousness to/for generation and generation till forever: enduring
32 Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
and be angry upon water Meribah and be evil to/for Moses in/on/with for the sake of them
33 kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
for to rebel [obj] spirit his and to speak rashly in/on/with lips his
34 Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
not to destroy [obj] [the] people which to say LORD to/for them
35 bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
and to pledge in/on/with nation and to learn: learn deed their
36 Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
and to serve: minister [obj] idol their and to be to/for them to/for snare
37 Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
and to sacrifice [obj] son: descendant/people their and [obj] daughter their to/for demon
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
and to pour: pour blood innocent blood son: descendant/people their and daughter their which to sacrifice to/for idol Canaan and to pollute [the] land: country/planet in/on/with blood
39 Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
and to defile in/on/with deed their and to fornicate in/on/with deed their
40 Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
and to be incensed face: anger LORD in/on/with people his and to abhor [obj] inheritance his
41 Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
and to give: give them in/on/with hand: power nation and to rule in/on/with them to hate them
42 Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
and to oppress them enemy their and be humble underneath: under hand: power their
43 Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
beat many to rescue them and they(masc.) to rebel in/on/with counsel their and to sink in/on/with iniquity: crime their
44 Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
and to see: see in/on/with distress to/for them in/on/with to hear: hear he [obj] cry their
45 kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
and to remember to/for them covenant his and to be sorry: relent like/as abundance (kindness his *Q(K)*)
46 Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
and to give: do [obj] them to/for compassion to/for face: before all to take captive them
47 Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
to save us LORD God our and to gather us from [the] nation to/for to give thanks to/for name holiness your to/for to praise in/on/with praise your
48 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.
to bless LORD God Israel from [the] forever: enduring and till [the] forever: enduring and to say all [the] people amen to boast: praise LORD

< Zaburi 106 >