< Zaburi 106 >
1 Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Hallelujah! Give thanks to the Lord for his goodness, for his kindness endures forever.
2 Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
Who can describe his heroic deeds, or publish all his praise?
3 Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
Happy they who act justly, and do righteousness evermore.
4 Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
Remember me, Lord, as you remember your people, and visit me with your gracious help.
5 ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
May I see the good fortune of your elect, may I share in the joy of your nation, and in the pride of your heritage.
6 Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
We, like our fathers, have sinned, we have done perversely and wickedly
7 Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
In the land of Egypt our fathers, all heedless of your wonders, and unmindful of your great kindness, at the Red Sea defied the Most High.
8 Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
But true to his name he saved them, in order to show his might.
9 Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
He rebuked the Red Sea, and it dried; they marched through the depths as through desert,
10 Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
saved from the hand of the hostile, redeemed from the hand of the foe.
11 Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
The waters covered their enemies: not one of them was left.
12 Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
So then they believed in his words, and began to sing his praise.
13 Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
But soon they forgot his deeds: they did not wait for his counsel.
14 Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
Their greed was ravenous in the desert; they put God to the test in the wilderness.
15 Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
He gave them the thing they had asked for, but sent wasting disease among them.
16 Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
The camp grew jealous of Moses and of Aaron, holy one of the Lord.
17 Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
The earth opened and swallowed up Dathan, and covered Abiram’s company.
18 Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
Fire broke out on their company, flame kindled upon the wicked.
19 Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
They made a calf in Horeb, and bowed to the molten image.
20 Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
They exchanged their glorious God for the image of ox that eats grass.
21 Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
They forgot the God who had saved them by mighty deeds in Egypt
22 miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
Wonders in the land of Ham, terrors by the Red Sea.
23 Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
So he vowed, and would have destroyed them, but for Moses his elect, who stepped into the breach before him, to divert his deadly wrath.
24 Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
They spurned the delightsome land, they refused to believe in his word.
25 Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
They grumbled in their tents, would not listen to the voice of the Lord.
26 Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
So he swore with uplifted hand to lay them low in the wilderness;
27 kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
to disperse their seed among heathen, to scatter them over the world.
28 Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
Then they joined them to Baal of Peor, and ate what was offered the dead.
29 Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
They provoked him to wrath by their deeds, and plague broke out among them.
30 Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
Then Phinehas stood between, and so the plague was stayed;
31 Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
and it was counted to him for righteousness unto all generations forever.
32 Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
They angered him at the waters of Meribah, through them it went ill with Moses.
33 kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
They rebelled against his spirit, and he uttered speech that was rash.
34 Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
They did not destroy the nations, as the Lord had commanded them;
35 bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
but they mingled with the heathen, and learned to do as they did.
36 Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
Their idol gods they worshipped, and they were ensnared by them.
37 Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
They sacrificed their sons and their daughters to the demons.
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
They poured out innocent blood the blood of their sons and daughters whom they offered to Canaan’s idols, and the land was polluted with blood.
39 Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
They became unclean by their works, and adulterous in their deeds.
40 Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
Then the Lord’s fury was on his people, filled with horror at his inheritance.
41 Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
He delivered them to the heathen, to the sway of those who hated them.
42 Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
Their enemies oppressed them, and subdued them under their hand.
43 Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
Many a time he saved them, but they rebelled at his counsel, and were brought low by their wrongdoing.
44 Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
Yet he looked upon their distress, when he heard their cry.
45 kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
He remembered his covenant, and, in his great kindness, relented.
46 Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
He caused them to be pitied by all who carried them captive.
47 Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
Save us, O Lord our God, and gather us out of the nations, to give thanks to your holy name, and to make our boast of your praise.
48 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.
Blessed be the Lord, the God of Israel, from everlasting to everlasting. And let all the people say “Amen.” Praise the Lord.