< Zaburi 106 >

1 Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Hallelujah. O give thanks unto the LORD; for He is good; for His mercy endureth for ever.
2 Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
Who can express the mighty acts of the LORD, or make all His praise to be heard?
3 Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
Happy are they that keep justice, that do righteousness at all times.
4 Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
Remember me, O LORD, when Thou favourest Thy people; O think of me at Thy salvation;
5 ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
That I may behold the prosperity of Thy chosen, that I may rejoice in the gladness of Thy nation, that I may glory with Thine inheritance.
6 Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
We have sinned with our fathers, we have done iniquitously, we have dealt wickedly.
7 Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
Our fathers in Egypt gave no heed unto Thy wonders; they remembered not the multitude of Thy mercies; but were rebellious at the sea, even at the Red Sea.
8 Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
Nevertheless He saved them for His name's sake, that He might make His mighty power to be known.
9 Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
And He rebuked the Red Sea, and it was dried up; and He led them through the depths, as through a wilderness.
10 Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
And He saved them from the hand of him that hated them, and redeemed them from the hand of the enemy.
11 Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
And the waters covered their adversaries; there was not one of them left.
12 Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
Then believed they His words; they sang His praise.
13 Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
They soon forgot His works; they waited not for His counsel;
14 Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
But lusted exceedingly in the wilderness, and tried God in the desert.
15 Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
And He gave them their request; but sent leanness into their soul.
16 Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
They were jealous also of Moses in the camp, and of Aaron the holy one of the LORD.
17 Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
The earth opened and swallowed up Dathan, and covered the company of Abiram.
18 Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
And a fire was kindled in their company; the flame burned up the wicked.
19 Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
They made a calf in Horeb, and worshipped a molten image.
20 Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
Thus they exchanged their glory for the likeness of an ox that eateth grass.
21 Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
They forgot God their saviour, who had done great things in Egypt;
22 miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
Wondrous works in the land of Ham, terrible things by the Red Sea.
23 Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
Therefore He said that He would destroy them, had not Moses His chosen stood before Him in the breach, to turn back His wrath, lest He should destroy them.
24 Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
Moreover, they scorned the desirable land, they believed not His word;
25 Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
And they murmured in their tents, they hearkened not unto the voice of the LORD.
26 Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
Therefore He swore concerning them, that He would overthrow them in the wilderness;
27 kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
And that He would cast out their seed among the nations, and scatter them in the lands.
28 Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
They joined themselves also unto Baal of Peor, and ate the sacrifices of the dead.
29 Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
Thus they provoked Him with their doings, and the plague broke in upon them.
30 Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
Then stood up Phinehas, and wrought judgment, and so the plague was stayed.
31 Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
And that was counted unto him for righteousness, unto all generations for ever.
32 Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
They angered Him also at the waters of Meribah, and it went ill with Moses because of them;
33 kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
For they embittered his spirit, and he spoke rashly with his lips.
34 Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
They did not destroy the peoples, as the LORD commanded them;
35 bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
But mingled themselves with the nations, and learned their works;
36 Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
And they served their idols, which became a snare unto them;
37 Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
Yea, they sacrificed their sons and their daughters unto demons,
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
And shed innocent blood, even the blood of their sons and of their daughters, whom they sacrificed unto the idols of Canaan; and the land was polluted with blood.
39 Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
Thus were they defiled with their works, and went astray in their doings.
40 Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
Therefore was the wrath of the LORD kindled against His people, and He abhorred His inheritance.
41 Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
And He gave them into the hand of the nations; and they that hated them ruled over them.
42 Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
Their enemies also oppressed them, and they were subdued under their hand.
43 Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
Many times did He deliver them; but they were rebellious in their counsel, and sank low through their iniquity.
44 Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
Nevertheless He looked upon their distress, when He heard their cry;
45 kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
And He remembered for them His covenant, and repented according to the multitude of His mercies.
46 Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
He made them also to be pitied of all those that carried them captive.
47 Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
Save us, O LORD our God, and gather us from among the nations, that we may give thanks unto Thy holy name, that we may triumph in Thy praise.
48 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.
Blessed be the LORD, the God of Israel, from everlasting even to everlasting, and let all the people say: 'Amen.' Hallelujah.

< Zaburi 106 >