< Zaburi 106 >

1 Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Hallelujah! Give thanks to the LORD, for He is good; His loving devotion endures forever.
2 Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
Who can describe the mighty acts of the LORD or fully proclaim His praise?
3 Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
Blessed are those who uphold justice, who practice righteousness at all times.
4 Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
Remember me, O LORD, in Your favor to Your people; visit me with Your salvation,
5 ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
that I may see the prosperity of Your chosen ones, and rejoice in the gladness of Your nation, and give glory with Your inheritance.
6 Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
We have sinned like our fathers; we have done wrong and acted wickedly.
7 Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
Our fathers in Egypt did not grasp Your wonders or remember Your abundant kindness; but they rebelled by the sea, there at the Red Sea.
8 Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
Yet He saved them for the sake of His name, to make His power known.
9 Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
He rebuked the Red Sea, and it dried up; He led them through the depths as through a desert.
10 Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
He saved them from the hand that hated them; He redeemed them from the hand of the enemy.
11 Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
The waters covered their foes; not one of them remained.
12 Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
Then they believed His promises and sang His praise.
13 Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
Yet they soon forgot His works and failed to wait for His counsel.
14 Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
They craved intensely in the wilderness and tested God in the desert.
15 Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
So He granted their request, but sent a wasting disease upon them.
16 Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
In the camp they envied Moses, as well as Aaron, the holy one of the LORD.
17 Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
The earth opened up and swallowed Dathan; it covered the assembly of Abiram.
18 Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
Then fire blazed through their company; flames consumed the wicked.
19 Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
At Horeb they made a calf and worshiped a molten image.
20 Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
They exchanged their Glory for the image of a grass-eating ox.
21 Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
They forgot God their Savior, who did great things in Egypt,
22 miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
wondrous works in the land of Ham, and awesome deeds by the Red Sea.
23 Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
So He said He would destroy them— had not Moses His chosen one stood before Him in the breach to divert His wrath from destroying them.
24 Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
They despised the pleasant land; they did not believe His promise.
25 Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
They grumbled in their tents and did not listen to the voice of the LORD.
26 Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
So He raised His hand and swore to cast them down in the wilderness,
27 kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
to disperse their offspring among the nations and scatter them throughout the lands.
28 Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
They yoked themselves to Baal of Peor and ate sacrifices offered to lifeless gods.
29 Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
So they provoked the LORD to anger with their deeds, and a plague broke out among them.
30 Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
But Phinehas stood and intervened, and the plague was restrained.
31 Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
It was credited to him as righteousness for endless generations to come.
32 Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
At the waters of Meribah they angered the LORD, and trouble came to Moses because of them.
33 kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
For they rebelled against His Spirit, and Moses spoke rashly with his lips.
34 Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
They did not destroy the peoples as the LORD had commanded them,
35 bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
but they mingled with the nations and adopted their customs.
36 Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
They worshiped their idols, which became a snare to them.
37 Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
They sacrificed their sons and their daughters to demons.
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
They shed innocent blood— the blood of their sons and daughters, whom they sacrificed to the idols of Canaan, and the land was polluted with blood.
39 Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
They defiled themselves by their actions and prostituted themselves by their deeds.
40 Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
So the anger of the LORD burned against His people, and He abhorred His own inheritance.
41 Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
He delivered them into the hand of the nations, and those who hated them ruled over them.
42 Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
Their enemies oppressed them, and subdued them under their hand.
43 Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
Many times He rescued them, but they were bent on rebellion and sank down in their iniquity.
44 Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
Nevertheless He heard their cry; He took note of their distress.
45 kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
And He remembered His covenant with them, and relented by the abundance of His loving devotion.
46 Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
He made them objects of compassion to all who held them captive.
47 Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
Save us, O LORD our God, and gather us from the nations, that we may give thanks to Your holy name, that we may glory in Your praise.
48 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.
Blessed be the LORD, the God of Israel, from everlasting to everlasting. Let all the people say, “Amen!” Hallelujah!

< Zaburi 106 >