< Zaburi 106 >

1 Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Praise the LORD! Give thanks to the LORD, for he is good, for his loving kindness endures forever.
2 Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
Who can utter the mighty acts of the LORD, or fully declare all his praise?
3 Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
Blessed are those who keep justice. Blessed is one who does what is right at all times.
4 Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
Remember me, LORD, with the favor that you show to your people. Visit me with your salvation,
5 ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
that I may see the prosperity of your chosen, that I may rejoice in the gladness of your nation, that I may glory with your inheritance.
6 Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
We have sinned with our fathers. We have committed iniquity. We have done wickedly.
7 Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
Our fathers did not understand your wonders in Egypt. They did not remember the multitude of your loving kindnesses, but were rebellious at the sea, even at the Red Sea.
8 Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
Nevertheless he saved them for his name’s sake, that he might make his mighty power known.
9 Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
He rebuked the Red Sea also, and it was dried up; so he led them through the depths, as through a desert.
10 Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
He saved them from the hand of him who hated them, and redeemed them from the hand of the enemy.
11 Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
The waters covered their adversaries. There was not one of them left.
12 Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
Then they believed his words. They sang his praise.
13 Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
They soon forgot his works. They did not wait for his counsel,
14 Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
but gave in to craving in the desert, and tested God in the wasteland.
15 Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
He gave them their request, but sent leanness into their soul.
16 Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
They envied Moses also in the camp, and Aaron, the LORD’s saint.
17 Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
The earth opened and swallowed up Dathan, and covered the company of Abiram.
18 Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
A fire was kindled in their company. The flame burned up the wicked.
19 Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
They made a calf in Horeb, and worshiped a molten image.
20 Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
Thus they exchanged their glory for an image of a bull that eats grass.
21 Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
They forgot God, their Savior, who had done great things in Egypt,
22 miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
wondrous works in the land of Ham, and awesome things by the Red Sea.
23 Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
Therefore he said that he would destroy them, had Moses, his chosen, not stood before him in the breach, to turn away his wrath, so that he would not destroy them.
24 Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
Yes, they despised the pleasant land. They did not believe his word,
25 Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
but murmured in their tents, and did not listen to the LORD’s voice.
26 Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
Therefore he swore to them that he would overthrow them in the wilderness,
27 kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
that he would overthrow their offspring among the nations, and scatter them in the lands.
28 Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
They joined themselves also to Baal Peor, and ate the sacrifices of the dead.
29 Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
Thus they provoked him to anger with their deeds. The plague broke in on them.
30 Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
Then Phinehas stood up and executed judgment, so the plague was stopped.
31 Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
That was credited to him for righteousness, for all generations to come.
32 Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
They angered him also at the waters of Meribah, so that Moses was troubled for their sakes;
33 kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
because they were rebellious against his spirit, he spoke rashly with his lips.
34 Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
They did not destroy the peoples, as the LORD commanded them,
35 bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
but mixed themselves with the nations, and learned their works.
36 Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
They served their idols, which became a snare to them.
37 Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
Yes, they sacrificed their sons and their daughters to demons.
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
They shed innocent blood, even the blood of their sons and of their daughters, whom they sacrificed to the idols of Canaan. The land was polluted with blood.
39 Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
Thus they were defiled with their works, and prostituted themselves in their deeds.
40 Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
Therefore the LORD burned with anger against his people. He abhorred his inheritance.
41 Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
He gave them into the hand of the nations. Those who hated them ruled over them.
42 Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
Their enemies also oppressed them. They were brought into subjection under their hand.
43 Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
He rescued them many times, but they were rebellious in their counsel, and were brought low in their iniquity.
44 Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
Nevertheless he regarded their distress, when he heard their cry.
45 kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
He remembered for them his covenant, and repented according to the multitude of his loving kindnesses.
46 Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
He made them also to be pitied by all those who carried them captive.
47 Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
Save us, LORD, our God, gather us from among the nations, to give thanks to your holy name, to triumph in your praise!
48 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.
Blessed be the LORD, the God of Israel, from everlasting even to everlasting! Let all the people say, “Amen.” Praise the LORD!

< Zaburi 106 >