< Zaburi 106 >

1 Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Halelujah. Oslavujte Hospodina, nebo dobrý jest, nebo na věky milosrdenství jeho.
2 Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
Kdo může vymluviti nesmírnou moc Hospodinovu, a vypraviti všecku chválu jeho?
3 Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
Blahoslavení, kteříž ostříhají soudu, a činí spravedlnost každého času.
4 Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
Pamatuj na mne, Hospodine, pro milost k lidu svému, navštěv mne spasením svým,
5 ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
Abych užíval dobrých věcí s vyvolenými tvými, a veselil se veselím národu tvého, a chlubil se spolu s dědictvím tvým.
6 Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
Zhřešili jsme i s otci svými, neprávě jsme činili, a bezbožnost páchali.
7 Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
Otcové naši v Egyptě nerozuměli předivným skutkům tvým, aniž pamatovali na množství milosrdenství tvých, ale odporni byli při moři, při moři Rudém.
8 Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
A však vysvobodil je pro jméno své, aby v známost uvedl moc svou.
9 Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
Nebo přimluvil moři Rudému, a vyschlo; i provedl je skrze hlubiny, jako po poušti.
10 Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
A tak zachoval je od ruky toho, jenž jich nenáviděl, a vyprostil je z ruky nepřítele.
11 Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
V tom přikryly vody ty, kteříž je ssužovali, nezůstalo ani jednoho z nich.
12 Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
A ačkoli věřili slovům jeho, a zpívali chválu jeho,
13 Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
Však rychle zapomenuli na skutky jeho, a nečekali na radu jeho;
14 Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
Ale jati jsouce žádostí na poušti, pokoušeli Boha silného na pustinách.
15 Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
I dal jim, čehož se jim chtělo, a však dopustil hubenost na život jejich.
16 Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
Potom, když horlili proti Mojžíšovi v vojště, a Aronovi, svatému Hospodinovu,
17 Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
Otevřevši se země, požřela Dátana, a přikryla zběř Abironovu.
18 Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
A roznícen byl oheň na rotu jejich, plamen spálil bezbožníky.
19 Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
Udělali i tele na Orébě, a skláněli se slitině.
20 Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
A změnivše slávu svou v podobiznu vola, jenž jí trávu,
21 Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
Zapomněli na Boha silného, spasitele svého, kterýž činil veliké věci v Egyptě.
22 miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
A předivné v zemi Chamově, přehrozné při moři Rudém.
23 Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
Pročež řekl, že je vypléní, kdyby se byl Mojžíš, vyvolený jeho, nepostavil v té mezeře před ním, a neodvrátil prchlivosti jeho, aby nehubil.
24 Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
Za tím zošklivili sobě zemi žádanou, nevěříce slovu jeho.
25 Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
A repcíce v staních svých, neposlouchali hlasu Hospodinova.
26 Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
A protož pozdvihl ruky své proti nim, aby je rozmetal po poušti,
27 kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
A aby rozptýlil símě jejich mezi pohany, a rozehnal je do zemí.
28 Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
Spřáhli se také byli s modlou Belfegor, a jedli oběti mrch.
29 Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
A tak dráždili Boha skutky svými, až se na ně obořila rána,
30 Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
Až se postavil Fínes, a pomstu vykonal, i přetržena jest rána ta.
31 Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
Což jest mu počteno za spravedlnost od národu do pronárodu, a až na věky.
32 Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
Opět ho byli popudili při vodách sváru, až se i Mojžíšovi zle stalo pro ně.
33 kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
Nebo k hořkosti přivedli ducha jeho, a pronesl ji rty svými.
34 Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
K tomu nevyplénili ani národů těch, o kterýchž jim byl Hospodin poručil,
35 bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
Ale směšujíce se s těmi národy, naučili se skutkům jejich,
36 Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
A sloužili modlám jejich, kteréž jim byly osídlem.
37 Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
Obětovali zajisté syny své a dcery své ďáblům.
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
A vylili krev nevinnou, krev synů svých a dcer svých, kteréž obětovali trapidlům Kananejským, tak že poškvrněna jest země těmi vraždami.
39 Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
I zmazali se skutky svými, a smilnili činy svými.
40 Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
Protož rozpáliv se v prchlivosti Hospodin na lid svůj, v ošklivost vzal dědictví své.
41 Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
A vydal je v ruce pohanů. I panovali nad nimi ti, jenž je v nenávisti měli,
42 Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
A utiskali je nepřátelé jejich, tak že sníženi jsou pod ruku jejich.
43 Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
Mnohokrát je vysvobozoval, oni však popouzeli ho radou svou, pročež potlačeni jsou pro nepravost svou.
44 Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
A však patřil na úzkost jejich, a slyšel křik jejich.
45 kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
Nebo se rozpomenul na smlouvu svou s nimi, a želel toho podlé množství milosrdenství svých,
46 Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
Tak že naklonil k nim lítostí všecky, kteříž je u vězení drželi.
47 Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
Zachovej nás, Hospodine Bože náš, a shromažď nás z těch pohanů, abychom slavili jméno tvé svaté, a chlubili se v chvále tvé.
48 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.
Požehnaný Hospodin Bůh Izraelský od věků až na věky. Na to rciž všecken lid: Amen, Halelujah.

< Zaburi 106 >