< Zaburi 105 >
1 Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake, wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
Hvalite Jahvu, prizivajte mu ime, navješćujte među narodima djela njegova!
2 Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa, waambieni matendo yake yote ya ajabu.
Pjevajte mu, svirajte mu, pripovijedajte sva njegova čudesa!
3 Lishangilieni jina lake takatifu, mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.
Dičite se svetim imenom njegovim, neka se raduje srce onih što traže Jahvu!
4 Mtafuteni Bwana na nguvu zake, utafuteni uso wake siku zote.
Tražite Jahvu i njegovu snagu, tražite svagda njegovo lice!
5 Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya, miujiza yake na hukumu alizozitamka,
Sjetite se čudesa koja učini, njegovih čuda i sudova usta njegovih!
6 enyi wazao wa Abrahamu mtumishi wake, enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
Abrahamov rod sluga je njegov, sinovi Jakovljevi njegovi izabranici!
7 Yeye ndiye Bwana Mungu wetu, hukumu zake zimo duniani pote.
On je Jahve, Bog naš; po svoj su zemlji njegovi sudovi!
8 Hulikumbuka agano lake milele, neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,
On se uvijek sjeća svojega Saveza, riječi koju dade tisući naraštaja:
9 agano alilolifanya na Abrahamu, kiapo alichomwapia Isaki.
Saveza koji sklopi s Abrahamom i zakletve svoje Izaku.
10 Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri, kwa Israeli liwe agano la milele:
Ustanovi je kao zakon Jakovu, Izraelu vječni Savez,
11 “Nitakupa wewe nchi ya Kanaani kuwa sehemu utakayoirithi.”
govoreći: “Tebi ću dati kanaansku zemlju kao dio u baštinu vašu.”
12 Walipokuwa wachache kwa idadi, wachache sana na wageni ndani yake,
Kad ih još bješe malo na broju, vrlo malo, i kad bjehu pridošlice u njoj,
13 walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
išli su od naroda do naroda, iz jednoga kraljevstva k drugom narodu,
14 Hakuruhusu mtu yeyote awaonee; kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:
ali ne dopusti nikom da ih tlači, kažnjavaše zbog njih kraljeve:
15 “Msiwaguse niliowatia mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”
“Ne dirajte u moje pomazanike, ne nanosite zla mojim prorocima!”
16 Akaiita njaa juu ya nchi na kuharibu chakula chao chote,
I on pozva glad na zemlju, sve zalihe uništi krušne.
17 naye akatuma mtu mbele yao, Yosefu, aliyeuzwa kama mtumwa.
Pred njima čovjeka posla: Josip u ropstvo bijaše prodan.
18 Walichubua miguu yake kwa minyororo, shingo yake ilifungwa kwa chuma,
Sputaše uzama noge njegove, u gvožđe mu vrat staviše,
19 hadi yale aliyotangulia kusema yalipotimia, hadi neno la Bwana lilipomthibitisha.
dok se ne ispuni proroštvo njegovo, Jahvina ga riječ potvrdi.
20 Mfalme alituma watu wakamfungua, mtawala wa watu alimwachia huru.
Kralj naredi da ga driješe, narÄodÄa poglavar oslobodi njega.
21 Alimfanya mkuu wa nyumba yake, mtawala juu ya vyote alivyokuwa navyo,
Za domaćina ga stavi kući svojoj, za nadstojnika sveg imanja svoga,
22 kuwaelekeza wakuu wa mfalme apendavyo na kuwafundisha wazee wake hekima.
da velikaše njegove po volji uči i starce njegove mudrosti da vodi.
23 Kisha Israeli akaingia Misri, Yakobo akaishi kama mgeni katika nchi ya Hamu.
Tad Izrael u Egipat uđe, Jakov došljak bješe u Kamovoj zemlji.
24 Bwana aliwafanya watu wake kuzaana sana, akawafanya kuwa wengi sana kuliko adui zao,
Narod svoj umnoži veoma, učini ga jačim od dušmana.
25 ndiye aliigeuza mioyo yao iwachukie watu wake, wakatenda hila dhidi ya watumishi wake.
Okrenu im srce da zamrze narod njegov, da slugama njegovim opaki budu.
26 Akamtuma Mose mtumishi wake, pamoja na Aroni, aliyemchagua.
Mojsija posla, slugu svoga, Arona, kog odabra.
27 Walifanya ishara zake za ajabu miongoni mwao, miujiza yake katika nchi ya Hamu.
Činjahu među njima znake njegove i čudesa u Kamovoj zemlji.
28 Alituma giza na nchi ikajaa giza, kwani si walikuwa wameyaasi maneno yake?
Posla tmine, i smrknu se, al' prkosiše oni riječima njegovim.
29 Aligeuza maji yao kuwa damu, ikasababisha samaki wao kufa.
U krv im vode prometnu i pobi ribe njihove.
30 Nchi yao ilijaa vyura tele, ambao waliingia hadi kwenye vyumba vya kulala vya watawala wao.
Zemljom im žabe provrvješe, prodriješe i u dvore kraljevske.
31 Alisema, yakaja makundi ya mainzi, na viroboto katika nchi yao yote.
Reče, i muha roj doletje i komarci u sve kraje njine.
32 Alibadilisha mvua yao ikawa mvua ya mawe, yenye umeme wa radi nchini yao yote,
Mjesto kiše grÓad im dade, ognjene munje po njihovoj zemlji.
33 akaharibu mizabibu yao na miti ya tini, na akaangamiza miti ya nchi yao.
Udari im lozu i smokve, polomi stabla u krajima njinim.
34 Alisema, nzige wakaja, tunutu wasio na idadi,
Reče, i skakavci dođoše i bezbrojne gusjenice s njima.
35 wakala kila jani katika nchi yao, wakala mazao ya ardhi yao.
U zemlji im proždriješe svu bilinu, proždriješe rod njihovih njiva.
36 Kisha akawaua wazaliwa wote wa kwanza katika nchi yao, matunda ya kwanza ya ujana wao wote.
Pobi sve prvorođene u njihovoj zemlji, sve prvine snage njihove.
37 Akawatoa Israeli katika nchi wakiwa na fedha na dhahabu nyingi, wala hakuna hata mmoja kutoka kabila zao aliyejikwaa.
Izvede ih sa srebrom i zlatom; u plemenima njinim bolesnih ne bješe.
38 Misri ilifurahi walipoondoka, kwa sababu hofu ya Israeli ilikuwa imewaangukia.
Odlasku njihovu Egipat se obradova, jer ga od njih strah spopade.
39 Alitandaza wingu kama kifuniko, na moto kuwamulikia usiku.
Rasprostro je oblak kao pokrov i oganj da se obnoć sja.
40 Waliomba, naye akawaletea kware, akawashibisha kwa mkate wa mbinguni.
Zamoliše, i dovede prepelice, nebeskim ih kruhom tad nahrani.
41 Alipasua mwamba, maji yakabubujika, yakatiririka jangwani kama mto.
Hrid rascijepi, i provri voda, pustinjom poteče kao rijeka.
42 Kwa maana alikumbuka ahadi yake takatifu, aliyompa Abrahamu mtumishi wake.
Tad se sjeti svete riječi svoje što je zada sluzi svome Abrahamu.
43 Aliwatoa watu wake kwa furaha, wateule wake kwa kelele za shangwe,
Puk svoj s klicanjem izvede i s veseljem izabrane svoje.
44 akawapa nchi za mataifa, wakawa warithi wa mali wengine walikuwa wameitaabikia:
I dade im zemlje poganske, trud naroda baštiniše,
45 alifanya haya ili wayashike mausia yake na kuzitii sheria zake. Msifuni Bwana.
da čuvaju naredbe njegove i zakone da mu paze. Aleluja!