< Zaburi 104 >
1 Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
Bendice, alma mía, a Yavé. ¡Oh Yavé, ʼElohim mío, cuánto te has engrandecido! Estás cubierto de esplendor y majestad.
2 Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
Te cubres como con un manto de luz. Extiendes el cielo como una cortina.
3 na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
Él coloca sobre las aguas las vigas de sus altas moradas. Él convierte las nubes en su carroza. Él anda sobre las alas del viento.
4 Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
Él designa los vientos como sus mensajeros, Y las llamas de fuego, como sus ministros.
5 Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
Él estableció la tierra sobre sus cimientos Para que no sea sacudida.
6 Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
Le colocaste como una ropa el abismo. Las aguas estaban sobre las montañas.
7 Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
A tu reprensión huyeron, Se precipitaron al estruendo de tu trueno.
8 yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
Subieron las montañas, Bajaron los valles al lugar que estableciste para ellos.
9 Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
Les fijaste un límite que no traspasarán, De manera que no volverán a cubrir la tierra.
10 Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
Él envía manantiales por los valles. Ellos fluyen entre las montañas.
11 Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
Dan de beber a todas las bestias del campo. Mitigan su sed los asnos monteses.
12 Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
Junto a ellos habitan las aves del cielo. Elevan voces entre las ramas.
13 Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
Él riega las montañas desde sus altas cámaras. Con el fruto de las obras de Él está saciada la tierra.
14 Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
Él desarrolla el pasto para el ganado, Y la vegetación para el servicio del hombre De tal modo que saque alimento de la tierra,
15 divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
Y vino que alegra el corazón del hombre, El aceite para que brille su semblante Y el pan que sustenta la vida del hombre.
16 Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
Los árboles de Yavé beben su savia, Los cedros del Líbano que Él plantó,
17 Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
Donde las aves construyen sus nidos, La cigüeña, cuya casa está en los cipreses,
18 Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
Las altas montañas para las cabras monteses, Las peñas, madrigueras de los conejos.
19 Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
Él hizo la luna para las estaciones. El sol conoce el punto de su ocaso.
20 Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
Pones la oscuridad y es de noche. En ella corretean todos los animales del bosque.
21 Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
Los leoncillos rugen tras la presa Y buscan de ʼEL su comida.
22 Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
Al salir el sol se retiran Y se echan en sus guaridas.
23 Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
Sale el hombre a su trabajo, A su labor hasta el anochecer.
24 Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
¡Cuán innumerables son tus obras, oh Yavé! Hiciste todas ellas con sabiduría. La tierra está llena de tus posesiones.
25 Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
Ahí está el grande y ancho mar, Donde hay enjambre de incontables animales, Tanto pequeños como grandes.
26 Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
Allí navegan los barcos, [Y el ]cocodrilo que formaste para que juguetee en él.
27 Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
Todos ellos esperan en Ti Para que les des su comida en su tiempo.
28 Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
Les das, ellos recogen. Abres tu mano, Y se sacian con lo bueno.
29 Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
Ocultas tu rostro Y ellos se desmayan. Les retiras su aliento, Y ellos expiran y vuelven a su polvo.
30 Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
Envías tu aliento, Son creados, Y renuevas la superficie de la tierra.
31 Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
¡Sea la gloria de Yavé para siempre! ¡Que se alegre Yavé en sus obras!
32 yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
Él mira a la tierra, Y ella tiembla, Él toca las montañas, Y ellas humean.
33 Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
A Yavé cantaré en mi vida, Mientras tenga vida cantaré salmos a mi ʼElohim.
34 Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
Sea agradable a Él mi meditación. Yo me regocijaré en Yavé.
35 Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.
Sean exterminados de la tierra los pecadores Y los perversos dejen de ser. ¡Bendice, alma mía, a Yavé! ¡Alaben a YA!