< Zaburi 104 >

1 Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
Bemdize, ó alma minha, ao Senhor: Senhor Deus meu, tu és magnificentissimo, estás vestido de gloria e de magestade.
2 Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
Elle se cobre de luz como de um vestido, estende os céus como uma cortina.
3 na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
Põe nas aguas as vigas das suas camaras; faz das nuvens o seu carro, anda sobre as azas do vento.
4 Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
Faz dos seus anjos espiritos, dos seus ministros um fogo abrazador.
5 Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
Lançou os fundamentos da terra, para que não vacille em tempo algum.
6 Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
Tu a cobres com o abysmo, como com um vestido: as aguas estavam sobre os montes.
7 Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
Á tua reprehensão fugiram: á voz do teu trovão se apressaram.
8 yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
Sobem aos montes, descem aos valles, até ao logar que para ellas fundaste.
9 Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
Termo lhes pozeste, que não ultrapassarão, para que não tornem mais a cobrir a terra.
10 Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
Tu, que fazes sair as fontes nos valles, as quaes correm entre os montes.
11 Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
Dão de beber a todo o animal do campo; os jumentos montezes matam a sua sêde.
12 Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
Junto d'ellas as aves do céu terão a sua habitação, cantando entre os ramos.
13 Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
Elle rega os montes desde as suas camaras: a terra se farta do fructo das suas obras.
14 Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
Faz crescer a herva para as bestas, e a verdura para o serviço do homem, para fazer sair da terra o pão,
15 divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
E o vinho que alegra o coração do homem, e o azeite que faz reluzir o seu rosto, e o pão que fortalece o coração do homem.
16 Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
As arvores do Senhor fartam-se de seiva, os cedros do Libano que elle plantou,
17 Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
Onde as aves se aninham: emquanto á cegonha, a sua casa é nas faias.
18 Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
Os altos montes são um refugio para as cabras montezes, e as rochas para os coelhos.
19 Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
Designou a lua para as estações: o sol conhece o seu occaso.
20 Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
Ordenas a escuridão, e faz-se noite, na qual saem todos os animaes da selva.
21 Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
Os leõesinhos bramam pela preza, e de Deus buscam o seu sustento.
22 Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
Nasce o sol e logo se acolhem, e se deitam nos seus covis.
23 Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
Então sae o homem á sua obra e ao seu trabalho, até á tarde.
24 Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
Ó Senhor, quão variadas são as tuas obras! todas as coisas fizeste com sabedoria; cheia está a terra das tuas riquezas.
25 Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
Assim é este mar grande e muito espaçoso, onde ha reptis sem numero, animaes pequenos e grandes.
26 Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
Ali andam os navios; e o leviathan que formaste para n'elle folgar.
27 Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
Todos esperam de ti, que lhes dês o seu sustento em tempo opportuno.
28 Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
Dando-lh'o tu, elles o recolhem; abres a tua mão, e se enchem de bens.
29 Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
Escondes o teu rosto, e ficam perturbados: se lhes tiras o folego, morrem, e voltam para o seu pó.
30 Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
Envias o teu Espirito, e são creados, e assim renovas a face da terra.
31 Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
A gloria do Senhor durará para sempre: o Senhor se alegrará nas suas obras.
32 yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
Olhando elle para a terra, ella treme; tocando nos montes, logo fumegam.
33 Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
Cantarei ao Senhor emquanto eu viver; cantarei louvores ao meu Deus, emquanto eu tiver existencia.
34 Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
A minha meditação ácerca d'elle será suave: eu me alegrarei no Senhor.
35 Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.
Desçam da terra os peccadores, e os impios não sejam mais. Bemdize, ó alma minha, ao Senhor. Louvae ao Senhor.

< Zaburi 104 >