< Zaburi 104 >

1 Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
Teici To Kungu, mana dvēsele! Kungs, mans Dievs, Tu esi ļoti liels, ar augstību un godību aptērpies.
2 Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
Tu ģērbies gaišumā kā apģērbā; tu izklāj debesis kā telti.
3 na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
Tu ūdeņus augstībā sev lieci par grīdu, tu dari padebešus par saviem ratiem, tu staigā uz vēja spārniem.
4 Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
Tu dari vējus par Saviem eņģeļiem un uguns liesmas par Saviem sulaiņiem.
5 Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
Zemi Tu esi dibinājis uz viņas pamatiem, ka tā nešaubās ne mūžam.
6 Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
Ar jūras dziļumiem Tu to apsedzis kā ar apģērbu, ūdeņi stāvēja pār kalniem.
7 Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
No Taviem draudiem tie bēga, no Tava pērkona tie steidzās projām;
8 yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
Kalni cēlās un lejas nogrima tai vietā, ko Tu tām biji licis.
9 Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
Tu esi licis robežas, tās tie (ūdeņi) nepārkāps un zemi vairs neapklās.
10 Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
Tu izvadi avotus pa ielejām, ka tie tek starp kalniem.
11 Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
Tie dzirdina visus lauka zvērus, tur atdzeras meža ēzeļi.
12 Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
Pie tiem mīt debesputni, zaros tie dzied.
13 Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
Tu slapini kalnus no augšienes; ar augļiem, ko Tu radi, zeme top piepildīta.
14 Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
Tu liec zālei augt priekš lopiem un sējai cilvēkam par labu, lai nāk maize no zemes
15 divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
Un vīns, kas iepriecina cilvēka sirdi, ka viņa vaigs top skaistāks nekā no eļļas, un ka maize spēcina cilvēka sirdi.
16 Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
Tā Kunga koki top papilnam slacināti, ciedra koki uz Lībanus, ko Viņš ir dēstījis.
17 Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
Tur putni dara ligzdas un stārķi dzīvo uz priedēm.
18 Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
Augstie kalni ir priekš mežu kazām, klintis kalna āpšiem par patvērumu.
19 Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
Tu esi darījis mēnesi laikmetiem, saule zin savu noiešanu.
20 Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
Tu dari tumsu, ka nakts metās; tad kustās visi meža zvēri.
21 Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
Jaunie lauvas rūc pēc laupījuma, meklēdami savu barību no Dieva.
22 Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
Un kad saule lec, tad tie atkal aizbēg un apguļas savās alās.
23 Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
Tad cilvēks iziet pie sava darba, pie sava lauka darba līdz vakaram.
24 Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
Cik lieli ir Tavi darbi, ak Kungs! Tos visus Tu esi darījis ar gudrību, - zeme ir Tava padoma pilna.
25 Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
Redzi, jūra, liela un plata uz abējām pusēm! Tur mudžēt mudž neskaitāmā pulkā visādi zvēri, lieli, mazi.
26 Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
Tur iet lielas laivas un Levijatans, ko Tu esi radījis, tur dzīvoties.
27 Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
Tie visi uz Tevi gaida, ka Tu tiem barību dodi savā laikā.
28 Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
Kad Tu tiem dod, tad tie salasa; kad Tu Savu roku atveri, tad tie ar labumu top pieēdināti.
29 Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
Tu apslēpi Savu vaigu, tad tie iztrūkstas; Tu atņem viņiem dvašu, tad tie mirst un paliek atkal par pīšļiem.
30 Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
Tu sūti Savu Garu, tad tie top radīti, un Tu atjauno zemes ģīmi.
31 Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
Tā Kunga godība paliek mūžīgi; Tas Kungs priecājās par Saviem darbiem.
32 yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
Viņš uzlūko zemi, tad tā dreb; Viņš aizskar kalnus, tad tie kūp.
33 Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
Es dziedāšu Tam Kungam, kamēr es dzīvoju; es slavēšu savu Dievu ar dziesmām, kamēr šeit esmu.
34 Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
Manas domas Viņam lai patīk; es priecāšos iekš Tā Kunga.
35 Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.
Grēcinieki no zemes lai izzūd un bezdievīgo lai vairs nav. Teici To Kungu, mana dvēsele, Alleluja.

< Zaburi 104 >