< Zaburi 104 >

1 Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
Ipsi David. Benedic, anima mea, Domino: Domine Deus meus, magnificatus es vehementer. Confessionem et decorem induisti,
2 Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
amictus lumine sicut vestimento. Extendens cælum sicut pellem,
3 na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
qui tegis aquis superiora ejus: qui ponis nubem ascensum tuum; qui ambulas super pennas ventorum:
4 Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
qui facis angelos tuos spiritus, et ministros tuos ignem urentem.
5 Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
Qui fundasti terram super stabilitatem suam: non inclinabitur in sæculum sæculi.
6 Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
Abyssus sicut vestimentum amictus ejus; super montes stabunt aquæ.
7 Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
Ab increpatione tua fugient; a voce tonitrui tui formidabunt.
8 yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
Ascendunt montes, et descendunt campi, in locum quem fundasti eis.
9 Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
Terminum posuisti quem non transgredientur, neque convertentur operire terram.
10 Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
Qui emittis fontes in convallibus; inter medium montium pertransibunt aquæ.
11 Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
Potabunt omnes bestiæ agri; expectabunt onagri in siti sua.
12 Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
Super ea volucres cæli habitabunt; de medio petrarum dabunt voces.
13 Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
Rigans montes de superioribus suis; de fructu operum tuorum satiabitur terra:
14 Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
producens fœnum jumentis, et herbam servituti hominum, ut educas panem de terra,
15 divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
et vinum lætificet cor hominis: ut exhilaret faciem in oleo, et panis cor hominis confirmet.
16 Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
Saturabuntur ligna campi, et cedri Libani quas plantavit:
17 Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
illic passeres nidificabunt: herodii domus dux est eorum.
18 Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
Montes excelsi cervis; petra refugium herinaciis.
19 Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
Fecit lunam in tempora; sol cognovit occasum suum.
20 Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
Posuisti tenebras, et facta est nox; in ipsa pertransibunt omnes bestiæ silvæ:
21 Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
catuli leonum rugientes ut rapiant, et quærant a Deo escam sibi.
22 Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
Ortus est sol, et congregati sunt, et in cubilibus suis collocabuntur.
23 Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
Exibit homo ad opus suum, et ad operationem suam usque ad vesperum.
24 Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
Quam magnificata sunt opera tua, Domine! omnia in sapientia fecisti; impleta est terra possessione tua.
25 Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
Hoc mare magnum et spatiosum manibus; illic reptilia quorum non est numerus: animalia pusilla cum magnis.
26 Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
Illic naves pertransibunt; draco iste quem formasti ad illudendum ei.
27 Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
Omnia a te expectant ut des illis escam in tempore.
28 Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
Dante te illis, colligent; aperiente te manum tuam, omnia implebuntur bonitate.
29 Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
Avertente autem te faciem, turbabuntur; auferes spiritum eorum, et deficient, et in pulverem suum revertentur.
30 Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
Emittes spiritum tuum, et creabuntur, et renovabis faciem terræ.
31 Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
Sit gloria Domini in sæculum; lætabitur Dominus in operibus suis.
32 yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
Qui respicit terram, et facit eam tremere; qui tangit montes, et fumigant.
33 Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
Cantabo Domino in vita mea; psallam Deo meo quamdiu sum.
34 Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
Jucundum sit ei eloquium meum; ego vero delectabor in Domino.
35 Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.
Deficiant peccatores a terra, et iniqui, ita ut non sint. Benedic, anima mea, Domino.

< Zaburi 104 >