< Zaburi 104 >
1 Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
Anima mia, benedici l’Eterno! O Eterno, mio Dio, tu sei sommamente grande; sei vestito di splendore e di maestà.
2 Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
Egli s’ammanta di luce come d’una veste; distende i cieli come un padiglione;
3 na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
egli costruisce le sue alte stanze nelle acque; fa delle nuvole il suo carro, s’avanza sulle ali del vento;
4 Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
fa dei venti i suoi messaggeri, delle fiamme di fuoco i suoi ministri.
5 Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
Egli ha fondato la terra sulle sue basi; non sarà smossa mai in perpetuo.
6 Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
Tu l’avevi coperta dell’abisso come d’una veste, le acque s’erano fermate sui monti.
7 Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
Alla tua minaccia esse si ritirarono, alla voce del tuo tuono fuggirono spaventate.
8 yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
Le montagne sorsero, le valli s’abbassarono nel luogo che tu avevi stabilito per loro.
9 Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
Tu hai posto alle acque un limite che non trapasseranno; esse non torneranno a coprire la terra.
10 Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
Egli manda fonti nelle valli, ed esse scorrono fra le montagne;
11 Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
abbeverano tutte le bestie della campagna, gli asini selvatici vi si dissetano.
12 Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
Presso a quelle si riparano gli uccelli del cielo; di mezzo alle fronde fanno udir la loro voce.
13 Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
Egli adacqua i monti dall’alto delle sue stanze, la terra è saziata col frutto delle tue opere.
14 Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
Egli fa germogliar l’erba per il bestiame e le piante per il servizio dell’uomo, facendo uscir dalla terra il nutrimento,
15 divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
e il vino che rallegra il cuor dell’uomo, e l’olio che gli fa risplender la faccia, e il pane che sostenta il cuore dei mortali.
16 Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
Gli alberi dell’Eterno sono saziati, i cedri del Libano, ch’egli ha piantati.
17 Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
Gli uccelli vi fanno i loro nidi; la cicogna fa dei cipressi la sua dimora;
18 Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
le alte montagne son per i camosci, le rocce sono il rifugio de’ conigli.
19 Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
Egli ha fatto la luna per le stagioni; il sole conosce il suo tramonto.
20 Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
Tu mandi le tenebre e vien la notte, nella quale tutte le bestie delle foreste si mettono in moto.
21 Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
I leoncelli ruggono dietro la preda e chiedono il loro pasto a Dio.
22 Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
Si leva il sole, esse si ritirano e vanno a giacere nei loro covi.
23 Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
L’uomo esce all’opera sua e al suo lavoro fino alla sera.
24 Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
Quanto son numerose le tue opere, o Eterno! Tu le hai fatte tutte con sapienza; la terra è piena delle tue ricchezze.
25 Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
Ecco il mare, grande ed ampio, dove si muovon creature senza numero, animali piccoli e grandi.
26 Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
Là vogano le navi e quel leviatan che hai creato per scherzare in esso.
27 Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
Tutti quanti sperano in te che tu dia loro il lor cibo a suo tempo.
28 Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
Tu lo dài loro ed essi lo raccolgono; tu apri la mano ed essi son saziati di beni.
29 Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
Tu nascondi la tua faccia, essi sono smarriti; tu ritiri il loro fiato, ed essi muoiono e tornano nella loro polvere.
30 Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
Tu mandi il tuo spirito, essi sono creati, e tu rinnovi la faccia della terra.
31 Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
Duri in perpetuo la gloria dell’Eterno, si rallegri l’Eterno nelle opere sue!
32 yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
Egli riguarda la terra, ed essa trema; egli tocca i monti, ed essi fumano.
33 Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
Io canterò all’Eterno finché io viva; salmeggerò al mio Dio finché io esista.
34 Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
Possa la mia meditazione essergli gradita! Io mi rallegrerò nell’Eterno.
35 Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.
Spariscano i peccatori dalla terra, e gli empi non siano più! Anima mia, benedici l’Eterno. Alleluia.