< Zaburi 104 >

1 Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
Mon âme, bénis l'Éternel! Éternel, ô mon Dieu, tu es merveilleusement grand; Tu es revêtu de splendeur et de majesté.
2 Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
L'Éternel s'enveloppe de lumière comme d'un manteau; Il déploie les cieux comme une tente.
3 na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
Il construit au-dessus des eaux sa demeure inaccessible; Les nuages lui servent de char; Il s'avance sur les ailes du vent.
4 Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
Il fait des vents ses messagers. Et des flammes de feu ses serviteurs.
5 Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
Il a posé la terre sur ses fondements: Elle ne sera jamais ébranlée.
6 Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
Tu l'avais enveloppée de l'abîme comme d'un vêtement; Les eaux s'étaient arrêtées sur les montagnes:
7 Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
A ta menace, elles reculèrent! Au bruit de ton tonnerre, elles s'enfuirent épouvantées.
8 yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
Les montagnes s'élevèrent et les vallées s'abaissèrent, A la place que tu leur avais assignée.
9 Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
Tu as fixé à la mer une limite qu'elle ne franchira pas Elle ne reviendra plus couvrir la terre.
10 Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
Dieu envoie des sources dans les vallons, Et elles coulent entre les montagnes.
11 Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
Elles abreuvent toutes les bêtes des champs; Les ânes sauvages y étanchent leur soif.
12 Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
Les oiseaux du ciel habitent sur leurs bords, Et font retentir leurs chants dans le feuillage.
13 Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
Du haut de sa demeure, Dieu abreuve les montagnes; La terre se rassasie du fruit de ses oeuvres.
14 Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
Il fait germer l'herbe pour le bétail, Et les plantes pour l'usage de l'homme, Qui tire ainsi de la terre sa nourriture:
15 divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
Le vin qui réjouit le coeur de l'homme, Et qui, mieux que l'huile, fait resplendir son visage, Ainsi que le pain qui fortifie le coeur de l'homme.
16 Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
Les arbres de l'Éternel, les cèdres du Liban Qu'il a plantés, sont gonflés de sève.
17 Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
Les oiseaux y bâtissent leurs nids; La cigogne fait des cyprès sa demeure.
18 Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
Les hautes montagnes sont l'asile des chamois, Et les rochers servent de retraite aux gerboises.
19 Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
L'Éternel a fait la lune pour marquer les temps, Ainsi que le soleil qui connaît l'heure de son déclin.
20 Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
Tu répands les ténèbres, et la nuit vient: Alors tous les animaux des forêts se mettent en mouvement.
21 Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
Les jeunes lions rugissent après leur proie Et demandent à Dieu leur pâture.
22 Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
Puis le soleil se lève: ils se retirent, Et vont se coucher dans leurs tanières.
23 Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
Alors l'homme sort, pour se rendre à son ouvrage Et se livrer à son travail jusqu'au soir.
24 Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
Éternel, combien tes oeuvres sont nombreuses! Tu les as toutes faites avec sagesse; La terre est pleine de tes richesses.
25 Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
Voici encore la grande et vaste mer! Là fourmillent, sans nombre. Des animaux petits et grands.
26 Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
Là se promènent les navires. Et ce monstre marin que tu as créé pour se jouer dans les flots,
27 Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
Tous ces êtres attendent de toi Que tu leur donnes, en temps opportun, leur nourriture.
28 Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
Tu la leur donnes, et ils la recueillent; Tu ouvres ta main, et ils sont rassasiés de biens.
29 Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
Si tu caches ta face, ils sont éperdus; Si tu leur retires le souffle, ils expirent Et retournent dans leur poussière.
30 Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
S'ils reçoivent de nouveau ton souffle, ils revivent. Et tu renouvelles la face de la terre.
31 Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
Que la gloire de l'Éternel dure à toujours! Que l'Éternel se réjouisse de ses oeuvres!
32 yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
Il regarde la terre, et la voilà qui tremble; Il touche les montagnes, et elles se couvrent de fumée.
33 Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
Je chanterai à la gloire de l'Éternel, tant que je vivrai; Je psalmodierai en l'honneur de mon Dieu, tant que j'existerai.
34 Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
Puisse mon cantique lui être agréable! Je me réjouirai en l'Éternel.
35 Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.
Que les pécheurs disparaissent de la terre. Et que les méchants n'existent plus! Mon âme, bénis l'Éternel! Louez l'Éternel!

< Zaburi 104 >