< Zaburi 104 >

1 Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
Bless the LORD, O my soul. O LORD my God, thou art very great; thou art clothed with honor and majesty.
2 Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
Who coverest [thyself] with light as [with] a garment: who stretchest out the heavens like a curtain:
3 na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
Who layeth the beams of his chambers in the waters: who maketh the clouds his chariot: who walketh upon the wings of the wind:
4 Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
Who maketh his angels spirits; his ministers a flaming fire:
5 Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
[Who] laid the foundations of the earth, [that] it should not be removed for ever.
6 Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
Thou coveredst it with the deep as [with] a garment: the waters stood above the mountains.
7 Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
At thy rebuke they fled; at the voice of thy thunder they hasted away.
8 yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
They go up by the mountains; they go down by the valleys to the place which thou hast founded for them.
9 Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
Thou hast set a bound that they may not pass over; that they turn not again to cover the earth.
10 Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
He sendeth the springs into the valleys, [which] run among the hills.
11 Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
They give drink to every beast of the field: the wild asses quench their thirst.
12 Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
By them shall the fowls of the heaven have their habitation, [which] sing among the branches.
13 Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
He watereth the hills from his chambers: the earth is satisfied with the fruit of thy works.
14 Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
He causeth the grass to grow for the cattle, and herb for the service of man: that he may bring forth food out of the earth;
15 divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
And wine [that] maketh glad the heart of man, [and] oil to make [his] face to shine, and bread [which] strengtheneth man's heart.
16 Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
The trees of the LORD are full [of sap]; the cedars of Lebanon, which he hath planted;
17 Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
Where the birds make their nests: [as for] the stork, the fir-trees [are] her house.
18 Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
The high hills [are] a refuge for the wild goats; [and] the rocks for the conies.
19 Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
He appointeth the moon for seasons: the sun knoweth his going down.
20 Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
Thou makest darkness, and it is night: in which all the beasts of the forest do creep [forth].
21 Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
The young lions roar after their prey, and seek their food from God.
22 Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
The sun ariseth, they collect, and lay themselves down in their dens.
23 Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
Man goeth forth to his work and to his labor until the evening.
24 Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
O LORD, how manifold are thy works! in wisdom hast thou made them all: the earth is full of thy riches.
25 Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
[So is] this great and wide sea, in which [are] creeping animals innumerable, both small and great beasts.
26 Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
There go the ships: [there is] that leviathan, [which] thou hast made to play therein.
27 Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
These wait all upon thee; that thou mayest give [them] their food in due season.
28 Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
[That which] thou givest them, they gather: thou openest thy hand, they are filled with good.
29 Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
Thou hidest thy face, they are troubled: thou takest away their breath, they die, and return to their dust.
30 Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
Thou sendest forth thy spirit, they are created: and thou renewest the face of the earth.
31 Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
The glory of the LORD shall endure for ever: the LORD shall rejoice in his works.
32 yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
He looketh on the earth, and it trembleth: he toucheth the hills, and they smoke.
33 Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
I will sing to the LORD as long as I live: I will sing praise to my God while I have my being.
34 Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
My meditation of him shall be sweet: I will be glad in the LORD.
35 Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.
Let sinners be consumed out of the earth, and let the wicked be no more. Bless thou the LORD, O my soul. Praise ye the LORD.

< Zaburi 104 >