< Zaburi 104 >

1 Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
Bless the LORD, O my soul. O LORD my God, Thou art very great; Thou art clothed with glory and majesty.
2 Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
Who coverest Thyself with light as with a garment, who stretchest out the heavens like a curtain;
3 na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
Who layest the beams of Thine upper chambers in the waters, who makest the clouds Thy chariot, who walkest upon the wings of the wind;
4 Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
Who makest winds Thy messengers, the flaming fire Thy ministers.
5 Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
Who didst establish the earth upon its foundations, that it should not be moved for ever and ever;
6 Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
Thou didst cover it with the deep as with a vesture; the waters stood above the mountains.
7 Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
At Thy rebuke they fled, at the voice of Thy thunder they hasted away —
8 yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
The mountains rose, the valleys sank down — unto the place which Thou hadst founded for them;
9 Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
Thou didst set a bound which they should not pass over, that they might not return to cover the earth.
10 Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
Who sendest forth springs into the valleys; they run between the mountains;
11 Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
They give drink to every beast of the field, the wild asses quench their thirst.
12 Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
Beside them dwell the fowl of the heaven, from among the branches they sing.
13 Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
Who waterest the mountains from Thine upper chambers; the earth is full of the fruit of Thy works.
14 Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
Who causeth the grass to spring up for the cattle, and herb for the service of man; to bring forth bread out of the earth,
15 divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
And wine that maketh glad the heart of man, making the face brighter than oil, and bread that stayeth man's heart.
16 Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
The trees of the LORD have their fill, the cedars of Lebanon, which He hath planted;
17 Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
Wherein the birds make their nests; as for the stork, the fir-trees are her house.
18 Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
The high mountains are for the wild goats; the rocks are a refuge for the conies.
19 Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
Who appointedst the moon for seasons; the sun knoweth his going down.
20 Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
Thou makest darkness, and it is night, wherein all the beasts of the forest do creep forth.
21 Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
The young lions roar after their prey, and seek their food from God.
22 Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
The sun ariseth, they slink away, and couch in their dens.
23 Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
Man goeth forth unto his work and to his labour until the evening.
24 Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
How manifold are Thy works, O LORD! In wisdom hast Thou made them all; the earth is full of Thy creatures.
25 Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
Yonder sea, great and wide, therein are creeping things innumerable, living creatures, both small and great.
26 Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
There go the ships; there is leviathan, whom Thou hast formed to sport therein.
27 Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
All of them wait for Thee, that Thou mayest give them their food in due season.
28 Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
Thou givest it unto them, they gather it; Thou openest Thy hand, they are satisfied with good.
29 Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
Thou hidest Thy face, they vanish; Thou withdrawest their breath, they perish, and return to their dust.
30 Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
Thou sendest forth Thy spirit, they are created; and Thou renewest the face of the earth.
31 Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
May the glory of the LORD endure for ever; let the LORD rejoice in His works!
32 yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
Who looketh on the earth, and it trembleth; He toucheth the mountains, and they smoke.
33 Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
I will sing unto the LORD as long as I live; I will sing praise to my God while I have any being.
34 Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
Let my musing be sweet unto Him; as for me, I will rejoice in the LORD.
35 Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.
Let sinners cease out of the earth, and let the wicked be no more. Bless the LORD, O my soul. Hallelujah.

< Zaburi 104 >