< Zaburi 104 >

1 Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
Let every part of me praise the Lord! Lord my God, you are so great, clothed with majesty and splendor!
2 Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
You wear light as your clothing; you stretch out the fabric of the heavens.
3 na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
You place the roof-beams of your house in the rainclouds. You make the clouds your chariots. You ride on the wings of the wind.
4 Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
You make your angels winds, and your servants flames of fire.
5 Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
You set the earth on its foundations; it will never be shaken.
6 Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
It was clothed with ocean depths—the waters even covered the mountains—
7 Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
but at your command the waters fled; at the sound of your thunder they rushed away.
8 yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
The mountains rose up and the valleys sank down to where you had determined.
9 Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
You set a boundary for the oceans so they would not come back and cover the earth.
10 Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
You make springs flow into the streams, running down between the hills.
11 Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
They provide water for all the wild animals, and wild donkeys quench their thirst.
12 Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
Birds build their nests in trees along the streams, singing from among the leaves.
13 Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
You send down rain on the mountains from your home high above; you fill the earth with good things.
14 Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
You make the grass grow for the cattle, and plants for people to eat—crops produced by the earth for food,
15 divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
and wine to make them happy, olive oil to make their faces shine, and bread to make them strong.
16 Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
The Lord's trees are well-watered, the cedars of Lebanon that he planted.
17 Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
Sparrows make their nests there; herons make their homes in the tall trees.
18 Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
Wild goats live high in the mountains; hyraxes hide among the rocks.
19 Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
You made the moon to mark the months, and the sun knows when to set.
20 Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
You make darkness fall and the night comes, the time when the forest animals come out to hunt.
21 Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
The young lions roar as they seek their prey, looking for the food that God provides for them.
22 Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
When the sun rises they return to their dens to rest.
23 Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
Then people leave for work, working until the evening.
24 Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
Lord, how many different things you have made—all of them wisely created! The earth is full of your creatures.
25 Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
Consider the sea, deep and wide, full of all kinds of living things, large and small.
26 Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
Ships sail there, and Leviathan, that you made to play in it.
27 Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
All creatures look to you to give them food at the right time.
28 Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
When you provide it, they gather it up. You hand out food to them, and they are well-fed.
29 Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
When you turn away from them, they're terrified; when you take away their breath, they die and return to dust.
30 Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
When you send your breath, they are created, and life covers the earth again.
31 Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
May the Lord's glory last forever! The Lord is happy with all he has made.
32 yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
He only has to look at the earth and it trembles; mountains pour out smoke at his touch.
33 Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
I will sing to the Lord for as long as I live; I will sing praises to my God my whole life.
34 Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
May he be pleased with my thoughts because I am happy in the Lord.
35 Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.
Let sinners be destroyed from the earth; let the wicked cease to exist. Let every part of me praise the Lord!

< Zaburi 104 >