< Zaburi 104 >

1 Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
[A Psalm] of David. Bless the Lord, O my soul. O Lord my God, you are very great; you have clothed yourself with praise and honour:
2 Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
who do robe yourself with light as with a garment; spreading out the heaven as a curtain.
3 na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
Who covers his chambers with waters; who makes the clouds his chariot; who walks on the wings of the wind.
4 Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
Who makes his angels spirits, and his ministers a flaming fire.
5 Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
Who establishes the earth on her sure foundation: it shall not be moved for ever.
6 Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
The deep, as it were a garment, is his covering: the waters shall stand on the hills.
7 Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
At your rebuke they shall flee; at the voice of your thunder they shall be alarmed.
8 yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
They go up to the mountains, and down to the plains, to the place which you have founded for them.
9 Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
You have set a bound which they shall not pass, neither shall they turn again to cover the earth.
10 Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
He sends forth his fountains amongst the valleys: the waters shall run between the mountains.
11 Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
They shall give drink to all the wild beasts of the field: the wild asses shall take [of them] to [quench] their thirst.
12 Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
By them shall the birds of the sky lodge: they shall utter a voice out of the midst of the rocks.
13 Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
He waters the mountains from his chambers: the earth shall be satisfied with the fruit of your works.
14 Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
He makes grass to grow for the cattle, and green herb for the service of men, to bring bread out of the earth;
15 divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
and wine makes glad the heart of man, to make his face cheerful with oil: and bread strengthens man's heart.
16 Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
The trees of the plain shall be full [of sap]; [even] the cedars of Libanus which he has planted.
17 Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
There the sparrows will build their nests; and the house of the heron takes the lead amongst them.
18 Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
The high mountains are a refuge for the stags, [and] the rock for the rabbits.
19 Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
He appointed the moon for seasons: the sun knows his going down.
20 Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
You did make darkness, and it was night; in it all the wild beasts of the forest will be abroad:
21 Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
[even] young lions roaring for prey, and to seek meat for themselves from God.
22 Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
The sun arises, and they shall be gathered together, and shall lie down in their dens.
23 Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
Man shall go forth to his work, and to his labour till evening.
24 Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
How great are your works, O Lord! in wisdom have you wrought them all: the earth is filled with your creation.
25 Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
[So is] this great and wide sea: there are things creeping innumerable, small animals and great.
26 Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
There go the ships; [and] this dragon whom you have made to play in it.
27 Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
All wait upon you, to give them [their] food in due season.
28 Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
When you have given [it] them, they will gather [it]; and when you have opened your hand, they shall all be filled with good.
29 Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
But when you have turned away your face, they shall be troubled: you will take away their breath, and they shall fail, and return to their dust.
30 Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
You shall send forth your Spirit, and they shall be created; and you shall renew the face of the earth.
31 Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
Let the glory of the Lord be for ever: the Lord shall rejoice in his works;
32 yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
who looks upon the earth, and makes it tremble; who touches the mountains, and they smoke.
33 Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
I will sing to the Lord while I live; I will sing praise to my God while I exist.
34 Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
Let my meditation be sweet to him: and I will rejoice in the Lord.
35 Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.
Let the sinners fail from off the earth, and transgressors, so that they shall be no more. Bless the Lord, O my soul.

< Zaburi 104 >