< Zaburi 104 >

1 Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
Min sjæl, lov HERREN! HERRE min Gud, du er saare stor! Du er klædt i Højhed og Herlighed,
2 Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
hyllet i Lys som en Kappe! Himlen spænder du ud som et Telt;
3 na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
du hvælver din Højsal i Vandene, gør Skyerne til din Vogn, farer frem paa Vindens Vinger;
4 Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
Vindene gør du til Sendebud, Ildsluer til dine Tjenere!
5 Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
Du fæsted Jorden paa dens Grundvolde, aldrig i Evighed rokkes den;
6 Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
Verdensdybet hylled den til som en Klædning, Vandene stod over Bjerge.
7 Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
For din Trusel flyede de, skræmtes bort ved din Tordenrøst,
8 yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
for op ad Bjerge og ned i Dale til det Sted, du havde beredt dem;
9 Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
du satte en Grænse, de ej kommer over, saa de ikke igen skal tilhylle Jorden.
10 Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
Kilder lod du rinde i Dale, hen mellem Bjerge flød de;
11 Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
de læsker al Markens Vildt, Vildæsler slukker deres Tørst;
12 Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
over dem bygger Himlens Fugle, mellem Grenene lyder deres Kvidder.
13 Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
Fra din Højsal vander du Bjergene, Jorden mættes fra dine Skyer;
14 Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
du lader Græs gro frem til Kvæget og Urter til Menneskets Tjeneste, saa du frembringer Brød af Jorden
15 divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
og Vin, der glæder Menneskets Hjerte, og lader Ansigtet glinse af Olie, og Brødet skal styrke Menneskets Hjerte.
16 Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
HERRENS Træer bliver mætte, Libanons Cedre, som han har plantet,
17 Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
hvor Fuglene bygger sig Rede; i Cypresser har Storken sin Bolig.
18 Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
Højfjeldet er for Stenbukken, Klipperne Grævlingens Tilflugt.
19 Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
Du skabte Maanen for Festernes Skyld, Solen kender sin Nedgangs Tid;
20 Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
du sender Mørke, Natten kommer, da rører sig alle Skovens Dyr;
21 Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
de unge Løver brøler efter Rov, de kræver deres Føde af Gud.
22 Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
De sniger sig bort, naar Sol staar op, og lægger sig i deres Huler;
23 Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
Mennesket gaar til sit Dagværk, ud til sin Gerning, til Kvæld falder paa.
24 Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
Hvor mange er dine Gerninger, HERRE, du gjorde dem alle med Visdom; Jorden er fuld af, hvad du har skabt!
25 Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
Der er Havet, stort og vidt, der vrimler det uden Tal af Dyr, baade smaa og store;
26 Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
Skibene farer der, Livjatan, som du danned til Leg deri.
27 Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
De bier alle paa dig, at du skal give dem Føde i Tide;
28 Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
du giver dem den, og de sanker, du aabner din Haand, og de mættes med godt.
29 Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
Du skjuler dit Aasyn, og de forfærdes; du tager deres Aand, og de dør og vender tilbage til Støvet;
30 Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
du sender din Aand, og de skabes, Jordens Aasyn fornyer du.
31 Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
HERRENS Herlighed vare evindelig, HERREN glæde sig ved sine Værker!
32 yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
Et Blik fra ham, og Jorden skælver, et Stød fra ham, og Bjergene ryger.
33 Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
Jeg vil synge for HERREN, saa længe jeg lever, lovsynge min Gud, den Tid jeg er til.
34 Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
Min Sang være ham til Behag, jeg har min Glæde i HERREN.
35 Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.
Maatte Syndere svinde fra Jorden og gudløse ikke mer være til! Min Sjæl, lov HERREN! Halleluja!

< Zaburi 104 >