< Zaburi 102 >

1 Maombi ya mtu aliyechoka. Anapoteseka na kumimina malalamiko yake kwa Bwana. Ee Bwana, usikie maombi yangu, kilio changu cha kuomba msaada kikufikie.
دعای مسکین وقتی که پریشان حال شده، ناله خود را به حضور یهوه می‌ریزد ای خداوند دعای مرا بشنو، و فریادمن نزد تو برسد.۱
2 Usinifiche uso wako ninapokuwa katika shida. Unitegee sikio lako, ninapoita, unijibu kwa upesi.
در روز تنگی‌ام روی خود را از من مپوشان. گوش خود را به من فراگیر، و روزی که بخوانم مرا به زودی اجابت فرما.۲
3 Kwa kuwa siku zangu zinatoweka kama moshi, mifupa yangu inaungua kama kaa la moto.
زیرا روزهایم مثل دود تلف شد واستخوانهایم مثل هیزم سوخته گردید.۳
4 Moyo wangu umefifia na kunyauka kama jani, ninasahau kula chakula changu.
دل من مثل گیاه زده شده و خشک گردیده است زیراخوردن غذای خود را فراموش می‌کنم.۴
5 Kwa sababu ya kusononeka kwangu kwa uchungu, nimebakia ngozi na mifupa.
به‌سبب آواز ناله خود، استخوانهایم به گوشت من چسبیده است.۵
6 Nimekuwa kama bundi wa jangwani, kama bundi kwenye magofu.
مانند مرغ سقای صحرا شده، ومثل بوم خرابه‌ها گردیده‌ام.۶
7 Nilalapo sipati usingizi, nimekuwa kama ndege mpweke kwenye paa la nyumba.
پاسبانی می‌کنم ومثل گنجشک بر پشت بام، منفرد گشته‌ام.۷
8 Mchana kutwa adui zangu hunidhihaki, wale wanaonizunguka hutumia jina langu kama laana.
تمامی روز دشمنانم مرا سرزنش می‌کنند و آنانی که برمن دیوانه شده‌اند مرا لعنت می‌نمایند.۸
9 Ninakula majivu kama chakula changu na nimechanganya kinywaji changu na machozi
زیراخاکستر را مثل نان خورده‌ام و مشروب خود را بااشک آمیخته‌ام،۹
10 kwa sababu ya ghadhabu yako kuu, kwa maana umeniinua na kunitupa kando.
به‌سبب غضب و خشم توزیرا که مرا برافراشته و به زیر افکنده‌ای.۱۰
11 Siku zangu ni kama kivuli cha jioni, ninanyauka kama jani.
روزهایم مثل سایه زوال پذیر گردیده و من مثل گیاه پژمرده شده‌ام.۱۱
12 Lakini wewe, Ee Bwana, umeketi katika kiti chako cha enzi milele, sifa zako za ukuu zaendelea vizazi vyote.
لیکن تو‌ای خداوند جلوس فرموده‌ای تاابدالاباد! و ذکر تو تا جمیع نسل هاست!۱۲
13 Utainuka na kuihurumia Sayuni, kwa maana ni wakati wa kumwonyesha wema; wakati uliokubalika umewadia.
توبرخاسته، بر صهیون ترحم خواهی نمود زیراوقتی است که بر او رافت کنی و زمان معین رسیده است.۱۳
14 Kwa maana mawe yake ni ya thamani kwa watumishi wako, vumbi lake lenyewe hulionea huruma.
چونکه بندگان تو در سنگهای وی رغبت دارند و بر خاک او شفقت می‌نمایند.۱۴
15 Mataifa wataogopa jina la Bwana, wafalme wote wa dunia watauheshimu utukufu wako.
پس امتها از نام خداوند خواهند ترسید وجمیع پادشاهان جهان از کبریایی تو.۱۵
16 Kwa maana Bwana ataijenga tena Sayuni na kutokea katika utukufu wake.
زیراخداوند صهیون را بنا نموده، و در جلال خودظهور فرموده است.۱۶
17 Ataitikia maombi ya mtu mkiwa, wala hatadharau hoja yao.
به دعای مسکینان توجه نموده، و دعای ایشان را خوار نشمرده است.۱۷
18 Hili na liandikwe kwa ajili ya kizazi kijacho, ili taifa litakaloumbwa baadaye waweze kumsifu Bwana:
این برای نسل آینده نوشته می‌شود تا قومی که آفریده خواهند شد خداوند را تسبیح بخوانند.۱۸
19 “Bwana alitazama chini kutoka patakatifu pake palipo juu, kutoka mbinguni alitazama dunia,
زیرا که از بلندی قدس خودنگریسته، خداوند از آسمان بر زمین نظر افکنده است.۱۹
20 kusikiliza vilio vya uchungu vya wafungwa na kuwaweka huru wale waliohukumiwa kufa.”
تا ناله اسیران را بشنود و آنانی را که به موت سپرده شده‌اند آزاد نماید.۲۰
21 Kwa hiyo jina la Bwana latangazwa huko Sayuni na sifa zake katika Yerusalemu,
تا نام خداوندرا در صیهون ذکر نمایند و تسبیح او را دراورشلیم،۲۱
22 wakati mataifa na falme zitakapokusanyika ili kumwabudu Bwana.
هنگامی که قوم‌ها با هم جمع شوند وممالک نیز تا خداوند را عبادت نمایند.۲۲
23 Katika kuishi kwangu alivunja nguvu zangu, akafupisha siku zangu.
توانایی مرا در راه ناتوان ساخت و روزهای مرا کوتاه گردانید.۲۳
24 Ndipo niliposema: “Ee Mungu wangu, usinichukue katikati ya siku zangu; miaka yako inaendelea vizazi vyote.
گفتم‌ای خدای من مرا در نصف روزهایم برمدار. سالهای تو تا جمیع نسل‌ها است.۲۴
25 Hapo mwanzo uliweka misingi ya dunia, nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.
از قدیم بنیاد زمین را نهادی وآسمان‌ها عمل دستهای تو است.۲۵
26 Hizi zitatoweka, lakini wewe utadumu, zote zitachakaa kama vazi. Utazibadilisha kama nguo nazo zitaondoshwa.
آنها فانی می‌شوند، لیکن تو باقی هستی و جمیع آنها مثل جامه مندرس خواهند شد. و مثل ردا آنها راتبدیل خواهی کرد و مبدل خواهند شد.۲۶
27 Lakini wewe, U yeye yule, nayo miaka yako haikomi kamwe.
لیکن تو همان هستی و سالهای تو تمام نخواهد گردید.۲۷
28 Watoto wa watumishi wako wataishi mbele zako; wazao wao wataimarishwa mbele zako.”
فرزندان بندگانت باقی خواهند ماند و ذریت ایشان در حضور تو پایدار خواهند بود.۲۸

< Zaburi 102 >