< Zaburi 101 >

1 Zaburi ya Daudi. Nitaimba juu ya upendo wako na haki yako; kwako wewe, Ee Bwana, nitaimba sifa.
Psalm Davidov: Milost in pravico bodem pel, tebi, o Gospod, prepeval.
2 Nitazingatia kuishi maisha yasiyo na lawama: utakuja kwangu lini? Nitatembea nyumbani mwangu kwa moyo usio na lawama.
Zapazil bodem na poštenem potu, ko prideš k meni; neprestano bodem hodil v poštenosti svojega srca v hiši svoji.
3 Sitaweka mbele ya macho yangu kitu kiovu. Ninayachukia matendo ya watu wasio na imani; hawatashikamana nami.
Stavil si ne bodem pred óči stvari pregrešne; delo njih sovražim, ki zavijajo v stran, držalo se me ne bode.
4 Moyo wa ukaidi utakuwa mbali nami; nitajitenga na kila ubaya.
Izprijeno srce bode daleč od mene; hudega ne bodem poznal.
5 Kila amsingiziaye jirani yake kwa siri, huyo nitamnyamazisha; mwenye macho ya dharau na moyo wa kiburi huyo sitamvumilia.
Njega, ki pred menoj skrivno obrekuje bližnjega svojega, bodem iztrebil; človeka s prevzetnim očesom, srcem napihnenim ne bodem mogel trpeti.
6 Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi, ili waweze kuishi pamoja nami; yeye ambaye moyo wake hauna lawama atanitumikia.
Oči moje bodo se vpirale na resnične v deželi, da naj sedajo z menoj; kdor hodi po poštenem potu, on bode mi stregel.
7 Mdanganyifu hatakaa nyumbani mwangu, yeye asemaye kwa uongo hatasimama mbele yangu.
Stanoval ne bode v moji hiši, kdor dela zvijačo; kdor govori laž, ne bode obstal pred mojimi očmi.
8 Kila asubuhi nitawanyamazisha waovu wote katika nchi; nitamkatilia mbali kila mtenda mabaya kutoka mji wa Bwana.
Vsako jutro bodem iztrebil vse krivične iz dežele, da potrebim iz mesta Gospodovega vse, ki delajo krivico.

< Zaburi 101 >