< Zaburi 101 >
1 Zaburi ya Daudi. Nitaimba juu ya upendo wako na haki yako; kwako wewe, Ee Bwana, nitaimba sifa.
Psaume de David. Je veux chanter la bonté et la justice; C'est toi, ô Éternel, que je célébrerai.
2 Nitazingatia kuishi maisha yasiyo na lawama: utakuja kwangu lini? Nitatembea nyumbani mwangu kwa moyo usio na lawama.
Je m'appliquerai à suivre la voie de l'intégrité. Quand viendras-tu à moi? Je donnerai l'exemple d'une conduite intègre. Au sein de ma famille.
3 Sitaweka mbele ya macho yangu kitu kiovu. Ninayachukia matendo ya watu wasio na imani; hawatashikamana nami.
Je chasserai de mon esprit toute pensée coupable. J'ai en horreur les actes d'iniquité: Ils n'ont aucun attrait pour moi.
4 Moyo wa ukaidi utakuwa mbali nami; nitajitenga na kila ubaya.
Le coeur pervers s'éloignera de moi; Je ne connaîtrai point le mal.
5 Kila amsingiziaye jirani yake kwa siri, huyo nitamnyamazisha; mwenye macho ya dharau na moyo wa kiburi huyo sitamvumilia.
J'anéantirai celui qui parle en secret contre son prochain. Je ne supporterai pas le regard hautain. Ni le coeur enflé d'orgueil.
6 Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi, ili waweze kuishi pamoja nami; yeye ambaye moyo wake hauna lawama atanitumikia.
J'aurai les yeux sur les fidèles du pays, Pour les faire demeurer avec moi. Celui qui marche dans l'intégrité, celui-là me servira.
7 Mdanganyifu hatakaa nyumbani mwangu, yeye asemaye kwa uongo hatasimama mbele yangu.
Celui qui use de tromperie n'habitera pas dans ma maison; Celui qui profère le mensonge Ne subsistera pas devant mes yeux.
8 Kila asubuhi nitawanyamazisha waovu wote katika nchi; nitamkatilia mbali kila mtenda mabaya kutoka mji wa Bwana.
Chaque matin, je détruirai tous les méchants du pays, Afin que tous les ouvriers d'iniquité Disparaissent de la cité de l'Éternel.