< Zaburi 101 >

1 Zaburi ya Daudi. Nitaimba juu ya upendo wako na haki yako; kwako wewe, Ee Bwana, nitaimba sifa.
Psaume de David Je veux chanter la bonté et la justice; C'est toi, Yahweh, que je veux célébrer.
2 Nitazingatia kuishi maisha yasiyo na lawama: utakuja kwangu lini? Nitatembea nyumbani mwangu kwa moyo usio na lawama.
Je prendrai garde à la voie de l'innocence. — Quand viendras-tu à moi? — Je marcherai dans l'intégrité de mon cœur, au milieu de ma maison.
3 Sitaweka mbele ya macho yangu kitu kiovu. Ninayachukia matendo ya watu wasio na imani; hawatashikamana nami.
Je ne mettrai devant mes yeux aucune action mauvaise. Je hais la conduite perverse; elle ne s'attachera point à moi.
4 Moyo wa ukaidi utakuwa mbali nami; nitajitenga na kila ubaya.
Un cœur faux ne sera jamais le mien; je ne veux pas connaître le mal.
5 Kila amsingiziaye jirani yake kwa siri, huyo nitamnyamazisha; mwenye macho ya dharau na moyo wa kiburi huyo sitamvumilia.
Le détracteur qui déchire en secret son prochain, je l'exterminerai; L'homme au regard hautain et au cœur gonflé d'orgueil, je ne le supporterai pas.
6 Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi, ili waweze kuishi pamoja nami; yeye ambaye moyo wake hauna lawama atanitumikia.
J'aurai les yeux sur les hommes fidèles du pays, pour qu'ils demeurent auprès de moi; celui qui marche dans une voie intègre sera mon serviteur.
7 Mdanganyifu hatakaa nyumbani mwangu, yeye asemaye kwa uongo hatasimama mbele yangu.
Il n'aura point de place dans ma maison, celui qui agit avec fourberie; celui qui profère le mensonge ne subsistera pas devant mes yeux.
8 Kila asubuhi nitawanyamazisha waovu wote katika nchi; nitamkatilia mbali kila mtenda mabaya kutoka mji wa Bwana.
Chaque matin j'exterminerai tous les méchants du pays, afin de retrancher de la cité de Yahweh tous ceux qui commettent l'iniquité.

< Zaburi 101 >