< Zaburi 101 >
1 Zaburi ya Daudi. Nitaimba juu ya upendo wako na haki yako; kwako wewe, Ee Bwana, nitaimba sifa.
Un psaume de David. Je chanterai la bonté et la justice. A toi, Yahvé, je chanterai des louanges.
2 Nitazingatia kuishi maisha yasiyo na lawama: utakuja kwangu lini? Nitatembea nyumbani mwangu kwa moyo usio na lawama.
Je veillerai à mener une vie irréprochable. Quand viendras-tu me voir? Je marcherai dans ma maison avec un cœur irréprochable.
3 Sitaweka mbele ya macho yangu kitu kiovu. Ninayachukia matendo ya watu wasio na imani; hawatashikamana nami.
Je ne mettrai pas de choses viles devant mes yeux. Je déteste les actes des hommes sans foi. Ils ne s'accrocheront pas à moi.
4 Moyo wa ukaidi utakuwa mbali nami; nitajitenga na kila ubaya.
Un cœur pervers sera loin de moi. Je ne veux rien avoir à faire avec le mal.
5 Kila amsingiziaye jirani yake kwa siri, huyo nitamnyamazisha; mwenye macho ya dharau na moyo wa kiburi huyo sitamvumilia.
Je ferai taire celui qui calomnie secrètement son prochain. Je ne tolérerai pas celui qui est arrogant et prétentieux.
6 Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi, ili waweze kuishi pamoja nami; yeye ambaye moyo wake hauna lawama atanitumikia.
Mes yeux se porteront sur les fidèles du pays, pour qu'ils puissent habiter avec moi. Celui qui marche d'une manière parfaite, il me servira.
7 Mdanganyifu hatakaa nyumbani mwangu, yeye asemaye kwa uongo hatasimama mbele yangu.
Celui qui pratique la tromperie n'habitera pas dans ma maison. Celui qui dit des mensonges ne sera pas établi devant mes yeux.
8 Kila asubuhi nitawanyamazisha waovu wote katika nchi; nitamkatilia mbali kila mtenda mabaya kutoka mji wa Bwana.
Matin après matin, je détruirai tous les méchants du pays, pour exterminer de la cité de Yahvé tous les artisans de l'iniquité.