< Zaburi 101 >

1 Zaburi ya Daudi. Nitaimba juu ya upendo wako na haki yako; kwako wewe, Ee Bwana, nitaimba sifa.
Davidin Psalmi. Minä veisaan armosta ja oikeudesta: sinulle, Herra, minä veisaan.
2 Nitazingatia kuishi maisha yasiyo na lawama: utakuja kwangu lini? Nitatembea nyumbani mwangu kwa moyo usio na lawama.
Minä tahdon vaarin ottaa oikiasta tiestä, koskas minun tyköni tulet: minä tahdon vaeltaa sydämeni vakuudessa minun huoneessani.
3 Sitaweka mbele ya macho yangu kitu kiovu. Ninayachukia matendo ya watu wasio na imani; hawatashikamana nami.
En minä ota pahaa asiaa eteeni: minä vihaan väärintekiöitä, ja en salli heitä olla tykönäni.
4 Moyo wa ukaidi utakuwa mbali nami; nitajitenga na kila ubaya.
Nurja sydän olkoon minusta pois: en minä kärsi pahaa.
5 Kila amsingiziaye jirani yake kwa siri, huyo nitamnyamazisha; mwenye macho ya dharau na moyo wa kiburi huyo sitamvumilia.
Joka lähimmäistänsä salaa panettelee, sen minä hukutan: en minä kärsi ylpeitä ja röyhkeitä.
6 Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi, ili waweze kuishi pamoja nami; yeye ambaye moyo wake hauna lawama atanitumikia.
Minun silmäni katsovat uskollisia maan päällä, että he asuisivat minun tykönäni: joka vaeltaa oikialla tiellä, se pitää oleman minun palveliani.
7 Mdanganyifu hatakaa nyumbani mwangu, yeye asemaye kwa uongo hatasimama mbele yangu.
Petollisia ihmisiä en minä pidä huoneessani: ei valehteliat menesty minun tykönäni.
8 Kila asubuhi nitawanyamazisha waovu wote katika nchi; nitamkatilia mbali kila mtenda mabaya kutoka mji wa Bwana.
Varhain minä hukutan kaikki jumalattomat maasta, hävittääkseni kaikkia pahantekiöitä Herran kaupungista.

< Zaburi 101 >