< Zaburi 101 >

1 Zaburi ya Daudi. Nitaimba juu ya upendo wako na haki yako; kwako wewe, Ee Bwana, nitaimba sifa.
A Psalm of David. I will sing of mercy and judgment: to thee, O LORD, will I sing.
2 Nitazingatia kuishi maisha yasiyo na lawama: utakuja kwangu lini? Nitatembea nyumbani mwangu kwa moyo usio na lawama.
I will behave myself wisely in a perfect way. O when wilt thou come to me? I will walk within my house with a perfect heart.
3 Sitaweka mbele ya macho yangu kitu kiovu. Ninayachukia matendo ya watu wasio na imani; hawatashikamana nami.
I will set no wicked thing before my eyes: I hate the work of them that turn aside; it shall not cleave to me.
4 Moyo wa ukaidi utakuwa mbali nami; nitajitenga na kila ubaya.
A froward heart shall depart from me: I will not know a wicked [person].
5 Kila amsingiziaye jirani yake kwa siri, huyo nitamnyamazisha; mwenye macho ya dharau na moyo wa kiburi huyo sitamvumilia.
Whoever privily slandereth his neighbor, him will I cut off: him that hath a high look and a proud heart I will not suffer.
6 Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi, ili waweze kuishi pamoja nami; yeye ambaye moyo wake hauna lawama atanitumikia.
My eyes [shall be] upon the faithful of the land, that they may dwell with me: he that walketh in a perfect way, he shall serve me.
7 Mdanganyifu hatakaa nyumbani mwangu, yeye asemaye kwa uongo hatasimama mbele yangu.
He that worketh deceit shall not dwell within my house: he that telleth lies shall not tarry in my sight.
8 Kila asubuhi nitawanyamazisha waovu wote katika nchi; nitamkatilia mbali kila mtenda mabaya kutoka mji wa Bwana.
I will early destroy all the wicked of the land; that I may cut off all who practice wickedness from the city of the LORD.

< Zaburi 101 >