< Zaburi 101 >

1 Zaburi ya Daudi. Nitaimba juu ya upendo wako na haki yako; kwako wewe, Ee Bwana, nitaimba sifa.
[A Psalm by David.] I will sing of loving kindness and justice. To you, LORD, I will sing praises.
2 Nitazingatia kuishi maisha yasiyo na lawama: utakuja kwangu lini? Nitatembea nyumbani mwangu kwa moyo usio na lawama.
I will be careful to live a blameless life. When will you come to me? I will walk within my house with a blameless heart.
3 Sitaweka mbele ya macho yangu kitu kiovu. Ninayachukia matendo ya watu wasio na imani; hawatashikamana nami.
I will set no vile thing before my eyes. I hate the deeds of faithless men. They will not cling to me.
4 Moyo wa ukaidi utakuwa mbali nami; nitajitenga na kila ubaya.
A perverse heart will be far from me. I will have nothing to do with evil.
5 Kila amsingiziaye jirani yake kwa siri, huyo nitamnyamazisha; mwenye macho ya dharau na moyo wa kiburi huyo sitamvumilia.
I will silence whoever secretly slanders his neighbor. I won't tolerate one who is haughty and conceited.
6 Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi, ili waweze kuishi pamoja nami; yeye ambaye moyo wake hauna lawama atanitumikia.
My eyes will be on the faithful of the land, that they may dwell with me. He who walks in a perfect way, he will serve me.
7 Mdanganyifu hatakaa nyumbani mwangu, yeye asemaye kwa uongo hatasimama mbele yangu.
He who practices deceit won't dwell within my house. He who speaks falsehood won't be established before my eyes.
8 Kila asubuhi nitawanyamazisha waovu wote katika nchi; nitamkatilia mbali kila mtenda mabaya kutoka mji wa Bwana.
Morning by morning, I will destroy all the wicked of the land; to cut off all evildoers from the LORD's city.

< Zaburi 101 >