< Zaburi 101 >
1 Zaburi ya Daudi. Nitaimba juu ya upendo wako na haki yako; kwako wewe, Ee Bwana, nitaimba sifa.
A Psalme of David. I will sing mercie and iudgement: vnto thee, O Lord, will I sing.
2 Nitazingatia kuishi maisha yasiyo na lawama: utakuja kwangu lini? Nitatembea nyumbani mwangu kwa moyo usio na lawama.
I will doe wisely in the perfite way, till thou commest to me: I will walke in the vprightnes of mine heart in the middes of mine house.
3 Sitaweka mbele ya macho yangu kitu kiovu. Ninayachukia matendo ya watu wasio na imani; hawatashikamana nami.
I wil set no wicked thing before mine eyes: I hate the worke of them that fall away: it shall not cleaue vnto me.
4 Moyo wa ukaidi utakuwa mbali nami; nitajitenga na kila ubaya.
A froward heart shall depart from me: I will knowe none euill.
5 Kila amsingiziaye jirani yake kwa siri, huyo nitamnyamazisha; mwenye macho ya dharau na moyo wa kiburi huyo sitamvumilia.
Him that priuily slandereth his neighbour, wil I destroy: him that hath a proude looke and hie heart, I cannot suffer.
6 Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi, ili waweze kuishi pamoja nami; yeye ambaye moyo wake hauna lawama atanitumikia.
Mine eyes shalbe vnto the faithfull of the lande, that they may dwell with me: he that walketh in a perfite way, he shall serue me.
7 Mdanganyifu hatakaa nyumbani mwangu, yeye asemaye kwa uongo hatasimama mbele yangu.
There shall no deceitful person dwell within mine house: he that telleth lyes, shall not remaine in my sight.
8 Kila asubuhi nitawanyamazisha waovu wote katika nchi; nitamkatilia mbali kila mtenda mabaya kutoka mji wa Bwana.
Betimes will I destroy all the wicked of the land, that I may cut off all the workers of iniquitie from the Citie of the Lord.