< Zaburi 101 >

1 Zaburi ya Daudi. Nitaimba juu ya upendo wako na haki yako; kwako wewe, Ee Bwana, nitaimba sifa.
A Psalm of David. I will sing of Your loving devotion and justice; to You, O LORD, I will sing praises.
2 Nitazingatia kuishi maisha yasiyo na lawama: utakuja kwangu lini? Nitatembea nyumbani mwangu kwa moyo usio na lawama.
I will ponder the way that is blameless— when will You come to me? I will walk in my house with integrity of heart.
3 Sitaweka mbele ya macho yangu kitu kiovu. Ninayachukia matendo ya watu wasio na imani; hawatashikamana nami.
I will set no worthless thing before my eyes. I hate the work of those who fall away; it shall not cling to me.
4 Moyo wa ukaidi utakuwa mbali nami; nitajitenga na kila ubaya.
A perverse heart shall depart from me; I will know nothing of evil.
5 Kila amsingiziaye jirani yake kwa siri, huyo nitamnyamazisha; mwenye macho ya dharau na moyo wa kiburi huyo sitamvumilia.
Whoever slanders his neighbor in secret, I will put to silence; the one with haughty eyes and a proud heart, I will not endure.
6 Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi, ili waweze kuishi pamoja nami; yeye ambaye moyo wake hauna lawama atanitumikia.
My eyes favor the faithful of the land, that they may dwell with me; he who walks in the way of integrity shall minister to me.
7 Mdanganyifu hatakaa nyumbani mwangu, yeye asemaye kwa uongo hatasimama mbele yangu.
No one who practices deceit shall dwell in my house; no one who tells lies shall stand in my presence.
8 Kila asubuhi nitawanyamazisha waovu wote katika nchi; nitamkatilia mbali kila mtenda mabaya kutoka mji wa Bwana.
Every morning I will remove all the wicked of the land, that I may cut off every evildoer from the city of the LORD.

< Zaburi 101 >