< Zaburi 100 >

1 Zaburi ya shukrani. Mpigieni Bwana kelele za shangwe, dunia yote.
Salmo de louvor: Gritai de alegria ao SENHOR toda a terra!
2 Mwabuduni Bwana kwa furaha; njooni mbele zake kwa nyimbo za shangwe.
Servi ao SENHOR com alegria; vinde com alegre canto perante sua presença.
3 Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu. Yeye ndiye alituumba, sisi tu mali yake; sisi tu watu wake, kondoo wa malisho yake.
Sabei que o SENHOR é Deus; foi ele, e não nós, que nos fez seu povo, e ovelhas de seu pasto.
4 Ingieni malangoni mwake kwa shukrani na katika nyua zake kwa kusifu, mshukuruni yeye na kulisifu jina lake.
Entrai pelas portas dele com agradecimento, por seus pátios com canto de louvor; agradecei a ele, [e] bendizei o seu nome.
5 Kwa maana Bwana ni mwema na upendo wake wadumu milele; uaminifu wake unadumu kwa vizazi vyote.
Porque o SENHOR é bom, sua bondade [dura] para sempre; e a fidelidade dele [continua] de geração após geração.

< Zaburi 100 >