< Zaburi 100 >

1 Zaburi ya shukrani. Mpigieni Bwana kelele za shangwe, dunia yote.
Ein Lied, zur Danksagung. - Entgegenjauchze alle Welt dem Herrn!
2 Mwabuduni Bwana kwa furaha; njooni mbele zake kwa nyimbo za shangwe.
Verehrt den Herrn mit Fröhlichkeit! Mit Jubel tretet vor sein Angesicht!
3 Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu. Yeye ndiye alituumba, sisi tu mali yake; sisi tu watu wake, kondoo wa malisho yake.
Bekennt: Der Herr ist Gott! Erschaffen hat er uns, wir sind sein Eigen, sein Volk, die Schäflein seiner Weide.
4 Ingieni malangoni mwake kwa shukrani na katika nyua zake kwa kusifu, mshukuruni yeye na kulisifu jina lake.
Zu seinen Toren ziehet dankend ein, mit Lobgesang in seine Höfe! Ihm dankt! Lobpreiset seinen Namen!
5 Kwa maana Bwana ni mwema na upendo wake wadumu milele; uaminifu wake unadumu kwa vizazi vyote.
Denn gütig ist der Herr. Auf immer währet seine Huld und seine Treue für und für.

< Zaburi 100 >