< Zaburi 100 >

1 Zaburi ya shukrani. Mpigieni Bwana kelele za shangwe, dunia yote.
Shout for joy to Adonai, all you lands!
2 Mwabuduni Bwana kwa furaha; njooni mbele zake kwa nyimbo za shangwe.
Abad ·Serve· Adonai with gladness. Come before his presence with singing.
3 Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu. Yeye ndiye alituumba, sisi tu mali yake; sisi tu watu wake, kondoo wa malisho yake.
Know that Adonai, he is God. It is he who has made us, and we are his. We are his people, and the sheep of his pasture.
4 Ingieni malangoni mwake kwa shukrani na katika nyua zake kwa kusifu, mshukuruni yeye na kulisifu jina lake.
Enter into his gates with thanksgiving, into his courts with tehilahot ·praise songs·. Yadah ·Extend hands in thankful praise· to him, and bless his name.
5 Kwa maana Bwana ni mwema na upendo wake wadumu milele; uaminifu wake unadumu kwa vizazi vyote.
For Adonai is good. His chesed ·loving-kindness· endures forever, his faithfulness to all generations.

< Zaburi 100 >