< Zaburi 100 >

1 Zaburi ya shukrani. Mpigieni Bwana kelele za shangwe, dunia yote.
A Psalm of thanksgiving. Make a joyful noise to the LORD, all the earth.
2 Mwabuduni Bwana kwa furaha; njooni mbele zake kwa nyimbo za shangwe.
Serve the LORD with gladness; come into His presence with joyful songs.
3 Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu. Yeye ndiye alituumba, sisi tu mali yake; sisi tu watu wake, kondoo wa malisho yake.
Know that the LORD is God. It is He who made us, and we are His; we are His people, and the sheep of His pasture.
4 Ingieni malangoni mwake kwa shukrani na katika nyua zake kwa kusifu, mshukuruni yeye na kulisifu jina lake.
Enter His gates with thanksgiving and His courts with praise; give thanks to Him and bless His name.
5 Kwa maana Bwana ni mwema na upendo wake wadumu milele; uaminifu wake unadumu kwa vizazi vyote.
For the LORD is good, and His loving devotion endures forever; His faithfulness continues to all generations.

< Zaburi 100 >