< Zaburi 100 >
1 Zaburi ya shukrani. Mpigieni Bwana kelele za shangwe, dunia yote.
Een psalm bij het dankoffer. Juicht Jahweh ter eer, heel de aarde,
2 Mwabuduni Bwana kwa furaha; njooni mbele zake kwa nyimbo za shangwe.
Dient Jahweh met vreugde, Treedt jubelend voor zijn aangezicht.
3 Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu. Yeye ndiye alituumba, sisi tu mali yake; sisi tu watu wake, kondoo wa malisho yake.
Erkent het: Jahweh is God; Hij heeft ons gemaakt, Hem behoren wij toe, Als zijn volk en de kudde zijner weide.
4 Ingieni malangoni mwake kwa shukrani na katika nyua zake kwa kusifu, mshukuruni yeye na kulisifu jina lake.
Treedt zijn poorten met dankzegging binnen, Zijn voorhoven met jubelzang, Brengt Hem glorie, en zegent zijn Naam.
5 Kwa maana Bwana ni mwema na upendo wake wadumu milele; uaminifu wake unadumu kwa vizazi vyote.
Want Jahweh is goed, Zijn genade duurt eeuwig, Zijn trouw van geslacht tot geslacht!