< Zaburi 10 >

1 Kwa nini, Ee Bwana, unasimama mbali? Kwa nini unajificha wakati wa shida?
¿POR qué estás lejos, oh Jehová, y te escondes en el tiempo de la tribulación?
2 Katika kiburi chake, mwovu humtesa maskini, waovu na wanaswe katika hila wanazozitunga.
Con arrogancia el malo persigue al pobre: serán cogidos en los artificios que han ideado.
3 Hujivunia tamaa za moyo wake; humbariki mlafi na kumtukana Bwana.
Por cuanto se alaba el malo del deseo de su alma, y bendice al codicioso, [á quien] Jehová aborrece.
4 Katika kiburi chake, mwovu hamtafuti Mungu, katika mawazo yake yote hakuna nafasi ya Mungu.
El malo, por la altivez de su rostro, no busca [á Dios]: no hay Dios [en] todos sus pensamientos.
5 Njia zake daima hufanikiwa; hujivuna na amri zako ziko mbali naye, huwacheka kwa dharau adui zake wote.
Sus caminos son viciosos en todo tiempo: tus juicios [los tiene] muy lejos de su vista: echa bocanadas en [orden á] todos sus enemigos.
6 Anajisemea mwenyewe, “Hakuna kitakachonitikisa, daima nitakuwa na furaha, kamwe sitakuwa na shida.”
Dice en su corazón: No seré movido en ningún tiempo, ni jamás [me alcanzará] el infortunio.
7 Kinywa chake kimejaa laana, uongo na vitisho; shida na ubaya viko chini ya ulimi wake.
Llena está su boca de maldición, y de engaños y fraude: debajo de su lengua, vejación y maldad.
8 Huvizia karibu na vijiji; kutoka mafichoni huwanasa wasio na hatia, akivizia wapitaji.
Está en las guaridas de las aldeas: en los escondrijos mata al inocente: sus ojos están acechando al pobre.
9 Huvizia kama simba aliye mawindoni; huvizia kumkamata mnyonge, huwakamata wanyonge na kuwaburuza katika wavu wake.
Acecha en oculto, como el león desde su cama: acecha para arrebatar al pobre: arrebata al pobre trayéndolo á su red.
10 Mateka wake hupondwa, huzimia; wanaanguka katika nguvu zake.
Encógese, agáchase, y caen en sus fuerzas muchos desdichados.
11 Anajisemea mwenyewe, “Mungu amesahau, huficha uso wake na haoni kabisa.”
Dice en su corazón: Dios está olvidado, ha encubierto su rostro; nunca lo verá.
12 Inuka Bwana! Inua mkono wako, Ee Mungu. Usiwasahau wanyonge.
Levántate, oh Jehová Dios, alza tu mano, no te olvides de los pobres.
13 Kwa nini mtu mwovu anamtukana Mungu? Kwa nini anajiambia mwenyewe, “Hataniita nitoe hesabu?”
¿Por qué irrita el malo á Dios? En su corazón ha dicho que no [lo] inquirirás.
14 Lakini wewe, Ee Mungu, unaona shida na huzuni, umekubali kuyapokea mkononi mwako. Mhanga anajisalimisha kwako, wewe ni msaada wa yatima.
Tú [lo] tienes visto: porque tú miras el trabajo, y la vejación, para vengar[le] por tu mano: á ti se acoge el pobre, tú eres el amparo del huérfano.
15 Vunja mkono wa mtu mwovu na mbaya, mwite atoe hesabu ya maovu yake ambayo yasingejulikana.
Quebranta el brazo del malo: del maligno buscarás su maldad, hasta que ninguna halles.
16 Bwana ni Mfalme milele na milele, mataifa wataangamia watoke nchini mwake.
Jehová, Rey eterno y perpetuo; de su tierra fueron destruídas las gentes.
17 Unasikia, Ee Bwana, shauku ya wanaoonewa, wewe huwatia moyo, na kusikiliza kilio chao,
El deseo de los humildes oíste, oh Jehová: tú dispones su corazón, y haces atento tu oído;
18 ukiwatetea yatima na walioonewa, ili mwanadamu, ambaye ni udongo, asiogopeshe tena.
Para juzgar al huérfano y al pobre, á fin de que no vuelva más á hacer violencia el hombre de la tierra.

< Zaburi 10 >