< Zaburi 1 >
1 Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
Wohl dem, der nicht wandelt nach dem Rate der Gottlosen, noch tritt auf den Weg der Sünder, noch sitzt, da die Spötter sitzen;
2 Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
sondern seine Lust hat am Gesetz des HERRN und in seinem Gesetze forscht Tag und Nacht.
3 Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
Der ist wie ein Baum, gepflanzt an Wasserbächen, der seine Frucht bringt zu seiner Zeit und dessen Blätter nicht verwelken, und alles, was er macht, gerät wohl.
4 Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
Nicht so die Gottlosen; sondern sie sind wie Spreu, die der Wind zerstreut.
5 Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
Darum werden die Gottlosen nicht bestehen im Gericht, noch die Sünder in der Gemeinde der Gerechten;
6 Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.
denn der HERR kennt den Weg der Gerechten; aber der Gottlosen Weg führt ins Verderben.