< Zaburi 1 >

1 Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
Heureux l'homme qui n'est point allé au conseil des impies qui ne s'est pas arrêté dans la voie des pécheurs et ne s'est point assis dans la chaire de pestilence,
2 Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
Mais dont la volonté est conforme à la loi du Seigneur, et qui, nuit et jour, méditera sur cette loi.
3 Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
Il sera comme l'arbre planté au bord des eaux, et qui donnera son fruit en sa saison; ses feuilles ne tomberont jamais, et en toutes ses œuvres il prospérera.
4 Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
Ils ne sont pas ainsi les impies, ils ne sont pas ainsi; mais ils sont comme la paille que le vent balaie sur la face de la terre.
5 Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
C'est pourquoi les impies ne ressusciteront pas dans le jugement, ni les pécheurs dans l'assemblée des justes.
6 Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.
Car le Seigneur connaît la voie des justes; et la voie des pécheurs périra.

< Zaburi 1 >