< Zaburi 1 >

1 Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
Heureux l'homme qui ne marche pas dans le conseil des impies, qui ne se tient pas dans la voie des pécheurs, et qui ne s'assied pas dans la compagnie des moqueurs,
2 Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
mais qui a son plaisir dans la loi de Yahweh, et qui la médite jour et nuit!
3 Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
Il est comme un arbre planté près d'un cours d'eau, qui donne son fruit en son temps, et dont le feuillage ne se flétrit pas: tout ce qu'il fait réussit.
4 Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
Il n'en est pas ainsi des impies: ils sont comme la paille que chasse le vent.
5 Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
Aussi les impies ne resteront-ils pas debout au jour du jugement, ni les pécheurs dans l'assemblée des justes.
6 Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.
Car Yahweh connaît la voie du juste, mais la voie des pécheurs mène à la ruine.

< Zaburi 1 >