< Zaburi 1 >
1 Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
Happy are those who don't follow the advice of the wicked. They refuse to adopt the ways of sinful people, and they don't make fun of others.
2 Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
Instead they love to do what the law of the Lord says, and they think about it day and night.
3 Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
They're like trees growing by flowing rivers, producing fruit every season. Their leaves never wither, and they are successful in all they do.
4 Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
But it's not like that for the wicked! They are like chaff, blown away by the wind.
5 Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
For this reason the wicked will not survive the judgment—sinners have no place among those who live right.
6 Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.
For the Lord watches over those who follow the right way, but the way of the wicked leads to death.