< Zaburi 1 >
1 Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
Blessed is the man who does not walk in the counsel of the wicked, or set foot on the path of sinners, or sit in the seat of mockers.
2 Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
But his delight is in the Law of the LORD, and on His law he meditates day and night.
3 Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
He is like a tree planted by streams of water, yielding its fruit in season, whose leaf does not wither, and who prospers in all he does.
4 Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
Not so the wicked! For they are like chaff driven off by the wind.
5 Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
Therefore the wicked will not stand in the judgment, nor sinners in the assembly of the righteous.
6 Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.
For the LORD guards the path of the righteous, but the way of the wicked will perish.