< Mithali 9 >
1 Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
La sabiduría hizo su casa, levantando sus siete pilares.
2 Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
Ella ha puesto sus bestias gordas a la muerte; su vino está mixto, su mesa está lista.
3 Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
Ella ha enviado a sus sirvientas; su voz sale a los lugares más altos de la ciudad, diciendo:
4 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
Él que sea simple, que entre aquí; y al que no tiene sentido, ella dice:
5 Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
Ven, toma de mi pan y de mi vino mezclado.
6 Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
Renuncia a los simples y ten vida, y sige el camino del conocimiento.
7 “Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
El que enseña a un hombre de orgullo se avergüenza a sí mismo; el que corrige a un pecador recibe un mal nombre.
8 Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
No reprendas a un hombre orgulloso, o él te odiará; corrige a un hombre sabio, y tu serás querido por él.
9 Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
Da enseñanza a un hombre sabio, y él se hará más sabio; da entrenamiento a un hombre recto, y su aprendizaje se incrementará.
10 “Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
El temor del Señor es el comienzo de la sabiduría, y el conocimiento del Santo da una mente sabia.
11 Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
Porque en mí aumentarán tus días, y los años de tu vida serán largos.
12 Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
Si eres sabio, eres sabio para ti mismo; si tu corazón está lleno de orgullo, solo tendrás el dolor de ello.
13 Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
La mujer necia está llena de ruido; ella no tiene ningún sentido en absoluto.
14 Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
Sentada a la puerta de su casa, en los altos del pueblo,
15 akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
y clamando a los que pasan, yendo en su camino, dice:
16 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
Cualquiera que sea simple, que entre aquí; y al que es sin sentido, ella dice:
17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
La bebida tomada sin derecho es dulce, y la comida en secreto es agradable.
18 Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol )
Pero él no ve que los muertos están allí, que sus invitados están en los lugares profundos del inframundo. (Sheol )