< Mithali 9 >

1 Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
La sabiduría hizo su casa, levantando sus siete pilares.
2 Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
Ella ha puesto sus bestias gordas a la muerte; su vino está mixto, su mesa está lista.
3 Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
Ella ha enviado a sus sirvientas; su voz sale a los lugares más altos de la ciudad, diciendo:
4 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
Él que sea simple, que entre aquí; y al que no tiene sentido, ella dice:
5 Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
Ven, toma de mi pan y de mi vino mezclado.
6 Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
Renuncia a los simples y ten vida, y sige el camino del conocimiento.
7 “Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
El que enseña a un hombre de orgullo se avergüenza a sí mismo; el que corrige a un pecador recibe un mal nombre.
8 Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
No reprendas a un hombre orgulloso, o él te odiará; corrige a un hombre sabio, y tu serás querido por él.
9 Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
Da enseñanza a un hombre sabio, y él se hará más sabio; da entrenamiento a un hombre recto, y su aprendizaje se incrementará.
10 “Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
El temor del Señor es el comienzo de la sabiduría, y el conocimiento del Santo da una mente sabia.
11 Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
Porque en mí aumentarán tus días, y los años de tu vida serán largos.
12 Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
Si eres sabio, eres sabio para ti mismo; si tu corazón está lleno de orgullo, solo tendrás el dolor de ello.
13 Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
La mujer necia está llena de ruido; ella no tiene ningún sentido en absoluto.
14 Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
Sentada a la puerta de su casa, en los altos del pueblo,
15 akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
y clamando a los que pasan, yendo en su camino, dice:
16 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
Cualquiera que sea simple, que entre aquí; y al que es sin sentido, ella dice:
17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
La bebida tomada sin derecho es dulce, y la comida en secreto es agradable.
18 Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol h7585)
Pero él no ve que los muertos están allí, que sus invitados están en los lugares profundos del inframundo. (Sheol h7585)

< Mithali 9 >